Tuesday , 23 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Ruto, Kenyatta wakutana mara ya kwanza baada ya uchaguzi
KimataifaTangulizi

Ruto, Kenyatta wakutana mara ya kwanza baada ya uchaguzi

Spread the love

RAIS mteule William Ruto leo Jumatatu tarehe 12 Septemba, 2022, amekutana na rais anayeondoka madarakani Uhuru Kenyatta katika Ikulu ya Rais Jijini Nairobi. Anaripotui Mwandishi Wetu…(endelea)

Ruto aliwasili katika Ikulu ya rais saa kumi na kupokewa na mwenyeji wake Uhuru Kenyatta. Rais Mteule aliambatana na mkewe Rachel Ruto.

Hii ni mara ya kwanza kwa wawili hao kukutana tangu Wakenya waliposhiriki katika shughuli ya kupiga kura ili kumchagua rais mpya.

Wawili hao walitofautiana baada ya rais Uhuru Kenyatta kumuunga mkono kiongozi wa upinzani Raila odinga katika uchaguzi uliopita.

Mkutano wao unajiri siku moja kabla ya sherehe ya kumuapisha William Ruto kuwa rais mpya wa Kenya.

Takriban viongozi 20 wa mataifa mbalimbali wamethibitisha kuhudhuria sherehe hiyo hapo kesho Jumanne akiwemo rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan.

Ruto aliibuka mshindi katika uchaguzi wa urais baada ya kumshinda mpinzani wake Raila Odinga.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Rais Samia ataja mikakati ya kufikia trilioni 2 biashara Uturuki, Tz

Spread the loveWakati Tanzania na Uturuki zikidhamiria kuongeza kiwango cha biashara hadi...

Habari za SiasaTangulizi

Mpina ataka Waziri Majaliwa ajiuzulu, akosoa teuzi za mawaziri

Spread the love  MBUNGE wa Kisesa, Luhaga Mpina, amemtaka Waziri Mkuu, Kassim...

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Habari za SiasaTangulizi

Tanzania, Uturuki zanuia kukuza biashara, uwekezaji

Spread the loveSERIKALI za Tanzania na Uturuki zimekubaliana kuendeleza dhamira ya kuimarisha...

error: Content is protected !!