Sunday , 28 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Makada CCM 8 wapitishwa kuwania ubunge EALA
Habari za SiasaTangulizi

Makada CCM 8 wapitishwa kuwania ubunge EALA

Spread the love

WABUNGE wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) jana wamewachagua wagombea nane kati ya 26 watakaokwenda kugombea Ubunge wa Bunge la Afrika Mashariki (EALA) tarehe 22 Septemba, 2022 bungeni jijini Dodoma. Anaripoti Mwandishi Wetu (endelea).

Hatua hiyo imefikiwa baada ya Kamati Kuu ya CCM (CC) katika kikao kilichoketi jijini Dar es Salaam, chini ya Mwenyekiti wa CCM, Rais Samia Suluhu Hassan, tarehe 7 Septemba, 2022, kuteua na kupendekeza majina 26 ya makada hao ambao jana tarehe 10 Septemba, 2022 wamechujwa na wabunge wa CCM na kubakia nane.

Waliochaguliwa ni; Dk Ng’waru Maghembe, James Millya, Anar Kachwamba, Dk Shogo Mlozi, Angela Kizigha, Machamo Ali Machamo, Dk Abdulla Hasnuu Makame na Nadra Juma Mohamed.

Katika Bunge la Eala, Tanzania ina nafasi tisa na kati ya hizo nane ni za Chama Cha Mapinduzi na moja ya vyama vya upinzani.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Biteko aipongeza GGML kudhibiti vifo, majeruhi mahali pa kazi

Spread the loveNAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

Habari za Siasa

Askofu Shoo awataka ACT kupigania maslahi ya Taifa, wasikubali kuhongwa

Spread the loveALIYEKUWA Askofu Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri, Askofu...

Habari za Siasa

Biteko aagiza waajiri kudhibiti vifo mahali pa kazi

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde aibana kampuni kutimiza masharti ya mkataba

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameitaka Kampuni ya Xin Tai...

error: Content is protected !!