WABUNGE wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) jana wamewachagua wagombea nane kati ya 26 watakaokwenda kugombea Ubunge wa Bunge la Afrika Mashariki (EALA) tarehe 22 Septemba, 2022 bungeni jijini Dodoma. Anaripoti Mwandishi Wetu (endelea).
Hatua hiyo imefikiwa baada ya Kamati Kuu ya CCM (CC) katika kikao kilichoketi jijini Dar es Salaam, chini ya Mwenyekiti wa CCM, Rais Samia Suluhu Hassan, tarehe 7 Septemba, 2022, kuteua na kupendekeza majina 26 ya makada hao ambao jana tarehe 10 Septemba, 2022 wamechujwa na wabunge wa CCM na kubakia nane.
Waliochaguliwa ni; Dk Ng’waru Maghembe, James Millya, Anar Kachwamba, Dk Shogo Mlozi, Angela Kizigha, Machamo Ali Machamo, Dk Abdulla Hasnuu Makame na Nadra Juma Mohamed.
Katika Bunge la Eala, Tanzania ina nafasi tisa na kati ya hizo nane ni za Chama Cha Mapinduzi na moja ya vyama vya upinzani.
Leave a comment