Friday , 3 May 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa 10,000 wafariki vita ya Urusi, Ukraine
Kimataifa

10,000 wafariki vita ya Urusi, Ukraine

Spread the love

 

WATU takribani 10,000 wameripotiwa kufariki dunia nchini Ukraine, tangu ilipovamiwa kijeshi na Urusi mwishoni wa Februari, 2022, ambapo Umoja wa Mataifa (UN) umesema kati ya vifo hivyo, raia 4,700 Ukraine wamepoteza maisha. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa … (endelea).

Kwa mujibu wa mtandao wa BBC Swahili, vifo hivyo vimetokea kuanzia Februari hadi Juni mwaka huu, huku ukieleza kwamba takwimu hizo ni pungufu ikilinganishwa na idadi halisi ya vifo kutokana na changamoto ya ukosefu wa idadi kamili kutokana na mapigano ya kijeshi yanayoendelea.

Mkuu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Haki za Binadamu nchini Ukraine, Matilder Bogner, amesema raia waliofariki dunia walikuwa katika miji iliyozingirwa au inayogombaniwa kwa sababu walikosa huduma z matibabu na msongo wa mawazo.

Kwa mujibu wa uchambuzi uliofanywa na BBC Swahili, watu wengi wamepoteza maisha katika Mji Mkuu wa Ukraine, Kyiv, wakati ulipozingirwa na vikosi vya kijeshi vya Urusi.

Wakatri takwimu hizo zikitolewa, Msaidizi Mkuu wa Rais wa Ukraine, Volodymyr Zelensky, alisema wanajeshi wa taifa hilo kati ya 100 hadi 200, hupoteza maisha kila siku.

Pia, Urusi imesema imeua wanajeshi wa Ukraine zaidi ya 20,000, huku wanajeshi wake 1,351 wakipoteza maisha tangu vita hiyo ianze.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifa

Mwanamke Rwanda ataka kupambana tena na Kagame

Spread the loveKIONGOZI wa kihistoria wa upinzani nchini Rwanda, Victoire Ingabire Umuhoza,...

Habari MchanganyikoKimataifa

Ruto amteua Kahariri kuwa mkuu wa majeshi

Spread the loveRAIS wa Kenya, William Ruto, amemteua Jenerali Charles Muriu Kahariri,...

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

error: Content is protected !!