Thursday , 2 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Rais Samia awapongeza madaktari waliowatenganisha mapacha Muhimbili
Habari Mchanganyiko

Rais Samia awapongeza madaktari waliowatenganisha mapacha Muhimbili

Spread the love

 

RAIS Samia Suluhu Hassan, ameipongeza timu ya madaktari na wauguzi wa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili, waliofanikisha upasuaji wa kuwatenganisha mapacha waliokuwa wameungana, Rehema na Neema, huku akiwaombea watoto hao wapone haraka. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam…(endelea).

Rais Samia ametoa pongezi hizo leo Jumamosi, tarehe 2 Julai 2022, kupitia ukurasa wake wa Twitter, siku moja baada ya madaktari hao kufanya upasuaji.

“Nawapongeza madaktari na wauguzi wa Hospitali ya Taifa Muhimbili, kwa kufanikisha upasuaji wa kuwatenganisha watoto mapacha walioungana. Hii ni hatua muhimu katika utekelezaji wa mpango wa serikali kuboresha matibabu ya kibingwa. Nawaombea watoto Rehema na Neema wapone haraka,” ameandika Rais Samia.

Watoto hao mapacha, walikuwa wameungana sehemu ya kifua, tumbo na ini, ambapo walifanyiwa upasuaji kwa muda wa zaidi ya saa sita.

Kwa mujibu wa Daktari Bingwa wa Upasuaji wa Watoto katika hospitali hiyo, Dk. Zaitun Bokhari, amesema upasuaji wa mapacha hao ulifanywa na madaktari 12, ambao ni madaktari wa usingizi sita, wa kutenganisha ngozi wane, wa kuangalia mfumo wa watoto kama unakwenda vizuri wawili na wauguzi sita.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

NEMC yatoa elimu matumizi sahihi ya zebaki kwa wachimbaji

Spread the loveBARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC)...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Oryx gesi yagawa mitungi, majiko 100 kwa waandishi wa habari Dar

Spread the loveKAMPUNI ya Oryx Gesi Tanzania imegawa mitungi 100 ya gesi...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari MchanganyikoMichezo

Wanamichezo Mei Mosi wachangia wahitaji vitu vya mil. 11.5

Spread the loveWanamichezo wanaoshiriki Michezo ya Mei Mosi Taifa 2024 jijini Arusha...

error: Content is protected !!