Friday , 19 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Rais Samia awapongeza madaktari waliowatenganisha mapacha Muhimbili
Habari Mchanganyiko

Rais Samia awapongeza madaktari waliowatenganisha mapacha Muhimbili

Spread the love

 

RAIS Samia Suluhu Hassan, ameipongeza timu ya madaktari na wauguzi wa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili, waliofanikisha upasuaji wa kuwatenganisha mapacha waliokuwa wameungana, Rehema na Neema, huku akiwaombea watoto hao wapone haraka. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam…(endelea).

Rais Samia ametoa pongezi hizo leo Jumamosi, tarehe 2 Julai 2022, kupitia ukurasa wake wa Twitter, siku moja baada ya madaktari hao kufanya upasuaji.

“Nawapongeza madaktari na wauguzi wa Hospitali ya Taifa Muhimbili, kwa kufanikisha upasuaji wa kuwatenganisha watoto mapacha walioungana. Hii ni hatua muhimu katika utekelezaji wa mpango wa serikali kuboresha matibabu ya kibingwa. Nawaombea watoto Rehema na Neema wapone haraka,” ameandika Rais Samia.

Watoto hao mapacha, walikuwa wameungana sehemu ya kifua, tumbo na ini, ambapo walifanyiwa upasuaji kwa muda wa zaidi ya saa sita.

Kwa mujibu wa Daktari Bingwa wa Upasuaji wa Watoto katika hospitali hiyo, Dk. Zaitun Bokhari, amesema upasuaji wa mapacha hao ulifanywa na madaktari 12, ambao ni madaktari wa usingizi sita, wa kutenganisha ngozi wane, wa kuangalia mfumo wa watoto kama unakwenda vizuri wawili na wauguzi sita.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB Pesa Akaunti yawavutia wakaguzi wa ndani Afrika

Spread the loveUbunifu wa bidhaa bora wa Benki ya NMB pamoja na...

Habari Mchanganyiko

Carbon First, Ruangwa wasaini makubaliano ya biashara ya hewa ukaa

Spread the love  KAMPUNI ya Carbon First Tanzania Limited na Halmashauri ya...

Habari Mchanganyiko

CBE yawakumbuka wenye mahitaji maalum Jangwani

Spread the loveCHUO cha Elimu ya Biashara (CBE), kimetoa msaada mbalimbali na...

Habari Mchanganyiko

Mume auwa mke kwa kumchoma visu, ajisalimisha Polisi

Spread the loveJACKSON Kalamji (49), anashikiliwa na Jeshi la Polisi jijini Mwanza,...

error: Content is protected !!