Wednesday , 8 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Serikali kupunguza mrabaha kwenye dhahabu, makaa ya mawe
Habari za Siasa

Serikali kupunguza mrabaha kwenye dhahabu, makaa ya mawe

Madini ya dhahabu
Spread the love

 

SERIKALI ya Tanzania, inakusudia kupunguza viwango vya mrabaha wa madini ya dhahabu na makaa ya mawe, yanayozalishwa nchini, katika mwaka wa fedha wa 2022/23. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).

Taarifa hiyo imetolewa leo Jumanne, tarehe 14 Juni 2022, bungeni jijini Dodoma na Waziri wa Fedha na Mipango, Dk. Mwigulu Nchemba, akiwasilisha makadirio ya mapato na matumizi ya Serikali kwa mwaka 2022/23.

Dk. Nchemba amesema, wizara yake inapendekeza kufanya marekebisho kwenye Sheria ya Madini, ili kupunguza kiwango cha kutoza marabaha kutoka asilimia sita hadi nne, kwa dhahabu inayouzwa kwenye vituo vya kusafisha madini.

https://www.youtube.com/watch?v=031HQcTN_qs

“Lengo la hatua hii ni kuhakikisha kuwa vituo vilivyoanzishwa nchini vinapata malighafi ya kutosha kwa ajili ya kusafisha na hatimaye kuongeza ajira na mapato ya Serikali,” amesema Dk. Mwigulu.

Katika hatua nyingine, Dk. Mwigulu amesema, Serikali inakusudia kupunguza kiwango cha marabaha kutoka kwenye makaa ya mawe yanayotumika kama malighafi za kuzalisha nishati viwandani, kutoka asilimia tatu hadi moja.

“Lengo la hatua hii ni kupunguza gharama za uzalishaji viwandani, kuchochea uwekezaji zaidi na kukuza ajira,” amesema Dk. Mwigulu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Rais Samia: Matumizi ya nishati safi sio anasa, ladha ipo

Spread the loveRAIS Samia Suluhu Hassan amesema matumizi ya nishati safi kwa...

Habari za SiasaTangulizi

Samia: Kuanzia Agosti marufuku kutumia mkaa, kuni

Spread the loveRAIS Samia Suluhu Hassan amemuagiza Waziri wa Nchi, Ofisi ya...

Habari za SiasaTangulizi

Mwendokasi Kigogo – Segerea kujengwa awamu ya 5

Spread the loveNaibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (TAMISEMI), Festo Dugange...

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Rais Samia ni Mzanzibari: Shida Iko Wapi?

Spread the loveTAIFA linakabiliwa na upungufu wa fikra sahihi. Upungufu huu unaonekana...

error: Content is protected !!