Wednesday , 8 May 2024
Home Kitengo Michezo Simba, Azam FC hakuna mbabe, Yanga ubingwa njia nyeupe
MichezoTangulizi

Simba, Azam FC hakuna mbabe, Yanga ubingwa njia nyeupe

Spread the love

 

KLABU za Simba na Azam FC zimetoshana nguvu kwa sare ya mabao 1-1, kwenye mchezo wa mzunguko wa 24 wa Ligi Kuu Tanzania Bara. Anaripoti Kelvin Mwaipungu, Dar es Salaam … (endelea).

Mchezo huo uliopigwa kwenye Uwanja wa Azam Complex Chamazi, majira ya saa 1 usiku nakushuhudia Simba ikidondosha alama mbili muhimu katika harakati za kuwania ubingwa.

Kwenye mchezo huo Azam FC ilikuwa ya kwanza kupata bao kupitia kwa Rogders Kola dakika ya 37, kabla ya dakika saba baadae Nahodha wa Simba, John Raphael Bocco kuisawazishia bao hilo na kufanya mchezo huo kwenda mapumziko ya sare ya bao 1-1.

Kipindi cha pili kiliporejea timu hizo zilishambuliana kwa zamu katika nyakati tofauti, lakini hakuna iliyofanikiwa kuona lango la mwenzake kwa mara ya pili.

Kwa matokeo hayo Simba inaendelea kusalia kwenye nafasi ya pili wakiwa na pointi 50, ikiwa ni tofauti ya pointi 10 nyuma ya Yanga ambao ni vinara wa Ligi hiyo wakiwa na pointi 60.

Kwa sasa Yanga wanahitaji alama tisa sawa na michezo mitatu, ili kutangazwa kuwa mabingwa wapya wa Ligi Kuu Tanzania Bara kwa mara ya 28.

Mara baada ya mchezo huo kikosi cha Simba kitasafiri kuelekea mkoani Geita, ambapo siku ya Jumapili tarehe 22 Mei 2022, watashuka dimbani majira ya saa 10 jioni kuikabili Geita Gold.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoMichezo

Kengold wakabidhiwa kombe NBC Championship

Spread the loveMdhamini mkuu wa Ligi Daraja la Kwanza (NBC Championship) Benki...

Habari za SiasaTangulizi

Samia: Kuanzia Agosti marufuku kutumia mkaa, kuni

Spread the loveRAIS Samia Suluhu Hassan amemuagiza Waziri wa Nchi, Ofisi ya...

Habari za SiasaTangulizi

Mwendokasi Kigogo – Segerea kujengwa awamu ya 5

Spread the loveNaibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (TAMISEMI), Festo Dugange...

Michezo

Piga pesa na mechi za UEFA

Spread the love  HATIMAYE leo hii ndio kitaeleweka nani aende Nusu Fainali...

error: Content is protected !!