Thursday , 2 May 2024
Home Kitengo Maisha Afya 1,580 wapoteza maisha wakati wa kujifungua ndani ya mwaka mmoja
AfyaHabari za Siasa

1,580 wapoteza maisha wakati wa kujifungua ndani ya mwaka mmoja

Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu
Spread the love

 

WANAWAKE 1,580 wamepoteza maisha nchini Tanzania wakati wa kujifungua katika kipindi cha mwaka mmoja wa 2021. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).

Hayo yamebainishwa leo Jumatatu tarehe 16, Mei, 2022 na Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu, bungeni jijini Dodoma wakati akiwasilisha makadirio ya mapato na matumizi kwa mwaka 2022/23.

Ummy amesema idadi hiyo ni kwa mujibu wa takwimu zinazokusanywa katika vituo vya kutolea huduma za afya nchini.

Hata hivyo amesema takwimu hizo zinaonesha vifo vitokanavyo na uzazi vimeendelea kupungua kutoka vifo 1,640 mwaka 2020.

“Takwimu hizi hazijumuishi vifo vinavyotokea kwenye ngazi ya jamii, hata hivyo zinatuonyesha mwenendo wa kupungua vifo vitokanavyo na uzazi,” amesema Mwalimu.

Amesema kupitia tafiti mbalimbali zinazoendelea kufanyika ikiwa ni pamoja na Tanzania Demographic Health Survey iliyoanza kufanyika Septemba 2021, zitaonesha hali iliyofikiwa katika jitihada za kupunguza vifo vitokanavyo na uzazi. Matokeo ya utafiti huo yanatarajiwa kutoka mwezi Septemba 2022.

Waziri huyo amesema katika kipindi cha Julai 2021 hadi Machi 2022, wajawazito 1,340,239 walihudumiwa na watoa huduma wenye ujuzi, ikilinganishwa na wajawazito 851,040 waliohudhuria kliniki kipindi kama hicho mwaka 2020.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari za Siasa

Mavunde aomba bilioni 231.9 bajeti wizara ya madini

Spread the loveWAZIRI wa Madini, Anthony Mavunde leo Jumanne amewasilisha hotuba ya...

Habari za SiasaTangulizi

Lissu amjibu Fatma Karume kuhusu Rais Samia

Spread the love  MAKAMU Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)...

Habari za SiasaTangulizi

Dk. Slaa: Watanzania iungeni mkono Chadema uchaguzi 2025

Spread the loveMWANASIASA mkongwe nchini Tanzania, Dk. Wilbroad Slaa, amewataka watanzania wakiunge...

error: Content is protected !!