Sunday , 28 April 2024
Home Gazeti Habari Mbuge aliyefariki kuagwa bungeni J5, kuzikwa Ijumaa Rukwa
HabariTangulizi

Mbuge aliyefariki kuagwa bungeni J5, kuzikwa Ijumaa Rukwa

Spread the love

 

MWILI wa aliyekuwa Mbunge Viti Maalumu (CCM), Mkoa wa Rukwa nchini Tanzania, Irene Ndyamkama, utazikwa mkoani Rukwa, Ijumaa ya tarehe 29 Aprili 2022. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma…(endelea).

Taarifa hiyo imetolewa leo Jumatatu, tarehe 25 Aprili 2022, jijini Dodoma na Spika wa Bunge, Dk. Tulia Ackson bungeni kabla ya kuahirisha shughuli za Bunge kwa mujibu wa kanuni hadi Jumatano, tarehe 27 Aprili mwaka huu, kwa ajili ya maombolezo ya msiba huo.

Spika Tulia amesema, mwili wa Ndyamkama utaagwa na wabunge keshokutwa- Jumatano bungeni kisha utazikwa mkoani Katavi.

“Kufuatia msiba huu, taarifa za awali ni kwamba, mwili wa marehemu utaletwa bungeni Jumatano, tarehe 27 Aprili 2022 kwa ajili ya kuagwa, mazishi yanatarajiwa kufanyika Ijumaa, tarehe 29 Aprili 2022 mkoani Katavi. Taarifa kuhusu msiba huu na jinsi tutakavyomuaga zitatolewa,” amesema Spika Tulia.

Spika Tulia amesema, marehemu Ndyamkama alifariki dunia jana Jumapili akipatiwa matibabu katika Hospitali ya Tumbi, iliyoko wilayani Kibaha Mkoa wa Pwani, baada ya kuugua ghafla akiwa safarini kuelekea Dar es Salaam na kulazimika kupelekwa hospitalini hapo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoTangulizi

Jacob, Malisa waachiwa kwa masharti

Spread the love  JESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam,...

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za SiasaTangulizi

Samia awataka watanzania kudumisha muungano

Spread the loveRais wa Tanzania,Samia Suluhu Hassan amewataka Watanzania kuendeleza Muungano kwa...

error: Content is protected !!