Thursday , 28 March 2024
Home Gazeti Habari Mbuge aliyefariki kuagwa bungeni J5, kuzikwa Ijumaa Rukwa
HabariTangulizi

Mbuge aliyefariki kuagwa bungeni J5, kuzikwa Ijumaa Rukwa

Spread the love

 

MWILI wa aliyekuwa Mbunge Viti Maalumu (CCM), Mkoa wa Rukwa nchini Tanzania, Irene Ndyamkama, utazikwa mkoani Rukwa, Ijumaa ya tarehe 29 Aprili 2022. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma…(endelea).

Taarifa hiyo imetolewa leo Jumatatu, tarehe 25 Aprili 2022, jijini Dodoma na Spika wa Bunge, Dk. Tulia Ackson bungeni kabla ya kuahirisha shughuli za Bunge kwa mujibu wa kanuni hadi Jumatano, tarehe 27 Aprili mwaka huu, kwa ajili ya maombolezo ya msiba huo.

Spika Tulia amesema, mwili wa Ndyamkama utaagwa na wabunge keshokutwa- Jumatano bungeni kisha utazikwa mkoani Katavi.

“Kufuatia msiba huu, taarifa za awali ni kwamba, mwili wa marehemu utaletwa bungeni Jumatano, tarehe 27 Aprili 2022 kwa ajili ya kuagwa, mazishi yanatarajiwa kufanyika Ijumaa, tarehe 29 Aprili 2022 mkoani Katavi. Taarifa kuhusu msiba huu na jinsi tutakavyomuaga zitatolewa,” amesema Spika Tulia.

Spika Tulia amesema, marehemu Ndyamkama alifariki dunia jana Jumapili akipatiwa matibabu katika Hospitali ya Tumbi, iliyoko wilayani Kibaha Mkoa wa Pwani, baada ya kuugua ghafla akiwa safarini kuelekea Dar es Salaam na kulazimika kupelekwa hospitalini hapo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Mapya yaibuka wamasai waliohamishwa Ngorongoro kwenda Msomera

Spread the loveMAPYA yameibuka kuhusu zoezi la Serikali kuwahamisha kwa hiari wamasai...

Habari MchanganyikoTangulizi

Baba aomba msaada kuzika miili ya familia yake iliyofunga bila kula kuonana na Mungu

Spread the loveWAKATI Mamlaka nchini Kenya, ikiendelea kukabidhi miili ya watu waliofariki...

Habari za SiasaTangulizi

Makonda awapopoa wanaomtofautisha Magufuli na Samia

Spread the loveKATIBU wa Itikadi na Uenezi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM),...

Habari za SiasaTangulizi

Kifo cha Magufuli: Mabeyo ‘akaanga’ wenzake

Spread the loveNANI aliyetaka kupindisha Katiba, ili aliyekuwa Makamu wa Rais, Samia...

error: Content is protected !!