Thursday , 2 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Prof. Muhongo ataka Tanzania iwe na satelaiti yake
Habari Mchanganyiko

Prof. Muhongo ataka Tanzania iwe na satelaiti yake

Spread the love

MBUNGE wa Musoma Vijijini, Profesa Sospeter (CCM) ameshauri Serikali kufikiria kuwa na satelaiti yake kwaajili ya tafiti zake za masuala mbalimbali ya maendeleo. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Prof. Muhongo ametoa ushauri huo Bungeni leo Jumatatu tarehe 11 Aprili 2022 wakati akichangia hoja bajeti ya Ofisi ya Waziri Mkuu na Wizara zake.

Amebainisha maeneo matano yanayotakiwa kuwekewa mkazo kwenye masuala ya utafiti ikiwemo ya masuala ya sayansi na teknolojia ya anga.

“Tukitaka kilimo bora , uvuvi, utalii lazima twende kwenye space sayansi na teknolojia. Wengi wakisikia space wanadhani ni kitu kikubwa sana cha kutisha hapana.

“Na tunahitaji kuwa na satelaiti…Kenya wana satelaiti, Uganda watarusha moja mwaka huu, Zambia watarusha moja mwakani, Rwanda wanayo moja, Misri wanazo tisa, Nigeria wanazo saba,”

Ameshauri watafiti na vyuo vya Tanzania lazima waanzishe program za shahada zinazojielekeza katika tasnia hiyo.

“Satelaiti sio kitu cha ajabu, tunazihitaji kwenye mawasiliano na hata mambo yetu ya hali ya hewa na madhara mengine ambayo yanaweza yakatupata,” amesisitiza.

Amesema mwaka 2020 nchi ambayo ilitumia fedha nyingi kwenye utafiti ni Ubelgiji na Sweden ambazo zilitumia asiimia 3.5 ya GDP zao.

Amesema mwaka 2006 nchi za Kiafrika zilipitisha azimio kule Sudani la kutumia angalau asilimia 1 ya pato la Taifa kwenye mambo ya utafiti.

Nchi nyingi za Afrika hazijafika huko waliokaribia ni Afrika Kusini, Kenya na Senegali na wao wako asilimia 0.8, Tanzania tupo asilimia 0.5,” amesema Muhongo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

Equity Bank yaendelea kusotea mabilioni ya fedha mahakama rufani

Spread the loveBENKI za Equity ya Tanzania na Kenya, zimeendelea kupambana mahakamani...

Habari Mchanganyiko

NEMC yatoa elimu matumizi sahihi ya zebaki kwa wachimbaji

Spread the loveBARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC)...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Oryx gesi yagawa mitungi, majiko 100 kwa waandishi wa habari Dar

Spread the loveKAMPUNI ya Oryx Gesi Tanzania imegawa mitungi 100 ya gesi...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

error: Content is protected !!