Tuesday , 7 May 2024
Home Gazeti Habari Chama amfunika Mayele
HabariMichezo

Chama amfunika Mayele

Spread the love

KIUNGO wa klabu ya Simba Clatous Chama amechaguliwa kuwa mchezaji bora wa Ligi Kuu Tanzania Bara mwezi Machi kufuatia kuonesha kiwango bora akiwa na kikosi cha klabu ya Simba ambao ndio mabingwa watetezi wa taji hilo. Anaripoti Kelvin Mwaipungu…(endelea)

Chama ameshinda tuzo hiyo mara baada ya kumshinda mshambuliaji hatari wa klabu ya Yanga Fiston Mayele na Frank Kahole wa Mtibwa Sugar ambao aliingia nao fainali.

Mchezaji huyo ambaye ambaye alirejea ndani ya klabu ya Simba kwenye dirisha dogo la usajili, ndani ya Mwezi Machi alifanikiwa kuisadia klabu yake ya Simba kuibuka na ushindi katika michezo miwili na kufunga mabao mawili.

Fiston Mayele, mshambuliaji wa Yanga

Tuzo hiyo ya Chama inakluwa tuzo ya kwanza ya mchezaji bora wa Ligi kutoka ndani ya klabu ya Simba, toka kuanza kwa msimu mpya wa mashindano 2021/2022.

Kiungo huyo anakuwa mchezaji wa saba kutwaa tuzso hiyo toka kuanza kwa msimu mpya, huku wachezaji wengine waliofanikiwa kutwaa tuzo hiyo ni Saido Ntibazonkiza (Februari) na Fiston Mayele (Januari) wote wa Yanga, Reliants Lusajo wa Namungo (Desemba), Jeremiah Juma wa Prisons (Novemba), Feisal Salum wa Yanga (Oktoba) na Vitalis Mayanga wa Polisi Tanzania (Septemba).

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Piga pesa na mechi za UEFA

Spread the love  HATIMAYE leo hii ndio kitaeleweka nani aende Nusu Fainali...

Michezo

Idris Sultan anogesha msimu wa 3 wa Bridgerton

Spread the loveSTAA wa burudani kutoka ardhi ya Tanzania, Idris Sultan amenogesha...

Michezo

Ligi mbalimbali za pesa kuendelea leo

Spread the love JUMAPILI ya leo imekaa kipesa tuu yani baada ya...

Michezo

Usiishie kuangalia tu game za leo, piga na mkwanja na Meridianbet

Spread the love  LIGI mbalimbali barani ulaya zitarejea tena Jumamosi ya leo...

error: Content is protected !!