Sunday , 28 April 2024
Habari za Siasa

Bunge Live larejea

Spread the love

VIKAO vya Bunge la Tanzania vitaanza kurushwa mubashara kuanzia kesho Jumanne, tarehe 5 Aprili 2022. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma…(endelea).

Taarufa hiyo imetolewa leo Jumatatu, tarehe 4 Aprili 2022, jijini Dodoma na Katibu wa Bunge, Nenelwa Mwihambi, akitoa ratiba ya Mkutano wa Saba wa Bunge unaoanza kesho.

Mwihambi amesema vikao hivyo vitaanza kurushwa mbashara baada ya Kamati ya Uongozi ya Bunge, kuridhia kufuatia kukamilika kwa maboresho ya studio ya mhimili huo.

Katibu huyo wa Bunge, ameviomba vyombo vya habari kutenga muda kwa ajili ya kurusha vikao hivyo.

“Vituo vya redio, chaneli za Tv na mitandao ya kijamii, wanaotaka watachukua matangazo hayo kutoka kwenye studio zetu moja kwa moja. Lakini naomba muujulishe umma na wenye vyombo vya habari wapokee hilo jambo na watutengee muda kwenye vituo vyao moja kwa moja,” amesema Mwihambi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Biteko aipongeza GGML kudhibiti vifo, majeruhi mahali pa kazi

Spread the loveNAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

Habari za Siasa

Askofu Shoo awataka ACT kupigania maslahi ya Taifa, wasikubali kuhongwa

Spread the loveALIYEKUWA Askofu Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri, Askofu...

Habari za Siasa

Biteko aagiza waajiri kudhibiti vifo mahali pa kazi

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde aibana kampuni kutimiza masharti ya mkataba

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameitaka Kampuni ya Xin Tai...

error: Content is protected !!