VIKAO vya Bunge la Tanzania vitaanza kurushwa mubashara kuanzia kesho Jumanne, tarehe 5 Aprili 2022. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma…(endelea).
Taarufa hiyo imetolewa leo Jumatatu, tarehe 4 Aprili 2022, jijini Dodoma na Katibu wa Bunge, Nenelwa Mwihambi, akitoa ratiba ya Mkutano wa Saba wa Bunge unaoanza kesho.
Mwihambi amesema vikao hivyo vitaanza kurushwa mbashara baada ya Kamati ya Uongozi ya Bunge, kuridhia kufuatia kukamilika kwa maboresho ya studio ya mhimili huo.
Katibu huyo wa Bunge, ameviomba vyombo vya habari kutenga muda kwa ajili ya kurusha vikao hivyo.
“Vituo vya redio, chaneli za Tv na mitandao ya kijamii, wanaotaka watachukua matangazo hayo kutoka kwenye studio zetu moja kwa moja. Lakini naomba muujulishe umma na wenye vyombo vya habari wapokee hilo jambo na watutengee muda kwenye vituo vyao moja kwa moja,” amesema Mwihambi.
Leave a comment