MAOFISA Ughani nchini watamilikishwa pikipiki zinazotolewa na Serikali baada ya kuzitumia kwa miaka miwili katika kutoa huduma kwa wakulima. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea)
Hatua hiyo inakuja baada ya Rais Samia Suluhu Hassan leo Jumatatu tarehe 4 Aprili 2022 kuridhia ombi lilotolewa na Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe.
Awali Bashe alisema Serikali haiwezi kushindwa kununua pikipiki hizo kila baada ya miaka miwili hivyo ni vyema wakamilikishwa ili zinunuliwezingine.
Serikali imegawa jumla pikipiki 7000 kwa maofisa ughani ambapo leo Rais Samia amegawa pikipiki 6,700 na zingine 300 zilishatolewa.
Hata hivyo Rais Samia amesema pikipiki hizo zitamilikishwa tu kwa wale ambao wataonekana wametekeleza majukumu yao ipasavyo.
“Haitakuwa blanked kwamba tutawamilikisha, hapana. Tutapima kwa kazi mnazofanya, na tunaamni kwa kipindi hicho thamani ya kazi yenu itakuwa imezidi hiyo ya pikipiki” amesema Rais Samia.
Ameongeza kuwa hatua hiyo itawapa hari ya kufanya kazi na kuzitunza pikipiki hizo wakijua baada ya hapo watazimiliki wao.
Mbali na pikipiki pia Rais Samia amesema Serikali itagawa vipima udongo kwa halmashauri 143, kutoa simu janja pamoja na visanduku 3300 kwa maafisa ughani.
Ametumia fursa hiyokuwataka maofisa ughani kutumia vitendeakazi hivyokama ilivyokusudiwa kwa manufaa ya Taifa.
Leave a comment