Wednesday , 1 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mbowe, Kinana, Lipumba kujadili mkwamo katiba mpya
Habari za SiasaTangulizi

Mbowe, Kinana, Lipumba kujadili mkwamo katiba mpya

Spread the love

 

KITUO cha Demokrasia Tanzania (TCD), kimemuita Mwenyekiti wa Chama cha Chadema, Freeman Mbowe, Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi (CUF), Prof. Ibrahim Lipumba na Katibu Mkuu Mstaafu wa CCM, Abdulrahman Kinana wajadili sababu za mkwamo wa mchakato wa upatikanaji katiba mpya. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea).

Hayo yamesemwa jana Jumanne, na Mwenyekiti wa TCD, Zitto Kabwe akizungumza katika majadala wa nini kianze kupatikana kati ya tume huru ya uchaguzi na katiba mpya, uliofanyika mtandaoni na kuongozwa na Mwanaharakati Maria Sarungi.

Zitto amesema, vigogo hao wa siasa Tanzania, watatoa maoni yao hayo kwenye mkutano wa TCD, unaotarajiwa kufanyika mwishoni mwa Machi 2022, jijini Dodoma, ambapo Rais Samia Suluhu Hassan, atakuwa mgeni rasmi.

Zitto Kabwe, Kiongozi wa ACT Wazalendo na Mwenyekiti wa Kituo cha Demokrasia Tanzania (TCD)

Amesema, Mbowe na wenzake, wameitwa kujadili sababu za mkwamo huo, kwa kuwa walishiriki kwenye mchakato wa upatikanaji katiba mpya, uliofanyika 2014, ambao walihusishwa katika kupendekeza muda maalumu wa mchakato huo kukamilika.

“Kwenye mkutano tunaoufanya Dodoma mwishoni mwa mwezi wa TCD, kuna ajenda itakayozungumzwa kwa nusu siku, kuhusu minimum reforms, ambao tumewiata ni watu waliouwepo kwenye makubaliano ya 2014, Kinana, Mbowe na Lipumba,” amesema Zitto na kuongeza”

Waje watuambie tulikwamaa wapi na nini kifanyike kukwamua mchakato wa katiba. Kwa hiyo mchakati wa katiba lazima uwepo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari za Siasa

Mavunde aomba bilioni 231.9 bajeti wizara ya madini

Spread the loveWAZIRI wa Madini, Anthony Mavunde leo Jumanne amewasilisha hotuba ya...

Habari za SiasaTangulizi

Lissu amjibu Fatma Karume kuhusu Rais Samia

Spread the love  MAKAMU Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)...

Habari za SiasaTangulizi

Dk. Slaa: Watanzania iungeni mkono Chadema uchaguzi 2025

Spread the loveMWANASIASA mkongwe nchini Tanzania, Dk. Wilbroad Slaa, amewataka watanzania wakiunge...

error: Content is protected !!