Thursday , 18 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mbowe, Kinana, Lipumba kujadili mkwamo katiba mpya
Habari za SiasaTangulizi

Mbowe, Kinana, Lipumba kujadili mkwamo katiba mpya

Spread the love

 

KITUO cha Demokrasia Tanzania (TCD), kimemuita Mwenyekiti wa Chama cha Chadema, Freeman Mbowe, Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi (CUF), Prof. Ibrahim Lipumba na Katibu Mkuu Mstaafu wa CCM, Abdulrahman Kinana wajadili sababu za mkwamo wa mchakato wa upatikanaji katiba mpya. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea).

Hayo yamesemwa jana Jumanne, na Mwenyekiti wa TCD, Zitto Kabwe akizungumza katika majadala wa nini kianze kupatikana kati ya tume huru ya uchaguzi na katiba mpya, uliofanyika mtandaoni na kuongozwa na Mwanaharakati Maria Sarungi.

Zitto amesema, vigogo hao wa siasa Tanzania, watatoa maoni yao hayo kwenye mkutano wa TCD, unaotarajiwa kufanyika mwishoni mwa Machi 2022, jijini Dodoma, ambapo Rais Samia Suluhu Hassan, atakuwa mgeni rasmi.

Zitto Kabwe, Kiongozi wa ACT Wazalendo na Mwenyekiti wa Kituo cha Demokrasia Tanzania (TCD)

Amesema, Mbowe na wenzake, wameitwa kujadili sababu za mkwamo huo, kwa kuwa walishiriki kwenye mchakato wa upatikanaji katiba mpya, uliofanyika 2014, ambao walihusishwa katika kupendekeza muda maalumu wa mchakato huo kukamilika.

“Kwenye mkutano tunaoufanya Dodoma mwishoni mwa mwezi wa TCD, kuna ajenda itakayozungumzwa kwa nusu siku, kuhusu minimum reforms, ambao tumewiata ni watu waliouwepo kwenye makubaliano ya 2014, Kinana, Mbowe na Lipumba,” amesema Zitto na kuongeza”

Waje watuambie tulikwamaa wapi na nini kifanyike kukwamua mchakato wa katiba. Kwa hiyo mchakati wa katiba lazima uwepo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Tume huru ya uchaguzi yatangaza ajira watendaji daftari wapiga kura

Spread the love  TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC), imetangaza nafasi...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema yatangaza ruti awamu ya pili maandamano

Spread the love  CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimesema awamu ya...

Habari za Siasa

CCM yamkana mwenyekiti UVCCM aliyetaka wapinzani wapotezwe

Spread the love  CHAMA Cha Mapinduzi (CCM), kimejitenga na kauli ya mwenyekiti...

Habari za SiasaTangulizi

Rais Samia kutunukiwa udaktari wa heshima Uturuki

Spread the loveBaraza la Chuo Kikuu cha Ankara, ambacho ni cha pili...

error: Content is protected !!