Thursday , 25 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Urusi yajibu mapigo, yamuwekea vikwazo Rais Marekani
Kimataifa

Urusi yajibu mapigo, yamuwekea vikwazo Rais Marekani

Rais wa Urusi, Vladimir Putin
Spread the love

 

NCHI ya Urusi imemuwekea vikwazo vya kuingia nchini humo Rais wa Marekani, Joe Biden na maofisa wengine 12 wa Taifa hilo, ikiwa ni hatua ya kujibu mapigo dhidi ya vikwazo ilivyowekewa. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa … (endelea).

Tayari Mrekani imewawekea vikwazo viongozi 11 wa ulinzi wa Urusi.

Mbali na Urusi kuwazuia viongozi hao wa Marekani, Taifa hilo limetangaza kuzuia mali zao zilizomo nchini humo.

Kwa mujibu wa Mtandao wa BBC Swahili, taarifa ya vikwazo hivyo imetolewa jana Jumanne na Wizara ya Mambo ya Nje Urusi.

Ikizungumzia vikwazo ilivyowekewa nchi yake na mataifa ya nje ikiwemo Marekani, kufuatia hatua yake ya kuivamia kijeshi Ukraine.

Joe Biden, Rais wa Marekani

Mbali na Rais Biden, maofisa wengine wa Marekani waliowekewa vikwazo hivyo, ni Katibu wa Ikulu ya Marekani, Antony Blinken. Katibu wa Ulinzi, Lloyd Austin. Katibu wa Habari, Jen Psaki. Mwenyekiti wa Wakuu wa Wafanyakazi, Mark Milley.

Wengine waliowekewa vikwazo ni Mshauri wa Taifa hilo wa masuala ya Usalama, Jake Sullivan na naibu wake Daleep Singh. Mismamizi wa Shirika la Marekani la Maendeleo ya Kimataifa (USAID), Samantha Power. Naibu Katibu wa Hazina, Wally Adeyemo na Rais wa Benki ya Export-Import ya Mrakeni, Reta Jo Lewis.

Marekani ni miongoni mwa mataifa ya nje yaliyiwekea vikwazo vya kiuchumi Russia, ambapo mataifa ya magharibi yamemuwekea vikwazo Rais wa Urusi, Vladimir Putin. Waziri wa Mambo ya Nje, Sergei Lavron na Katibu wa Habari, Dmitry Peskov.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

Habari MchanganyikoKimataifa

Tetemeko la ardhi laua 7, lajeruhi 800 Taiwan

Spread the loveWatu wapatao saba wamefariki dunia na wengine zaidi ya 800...

error: Content is protected !!