Thursday , 2 May 2024
Home Habari Mchanganyiko DPP awafutia mashtaka ya ugaidi masheikh 15
Habari Mchanganyiko

DPP awafutia mashtaka ya ugaidi masheikh 15

Sylivester Mwakitalu, Mkurugenzi wa Mashtaka nchini (DPP)
Spread the love

 

MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu, jijini Dar es Salaam, imewaacha huru Masheikh 15, baada ya Mkurugenzi wa Mashtaka nchini (DPP), Sylvester Mwakitalu kutokuwa na nia ya kuendelea na mashtaka ya ugaidi yaliyokuwa yanawakabili. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Msemaji wa Shuraa ya Maimamu, Ibrahim Mkondo, Masheikh hao waliachwa huru, jana tarehe 1 Machi 2022, baada ya kusota mahabusu kwa miaka saba.

“Mkurugenzi wa Mashtaka amewafutia mashtaka ya ugaidi watu 15, jijini Dar es Salaam leo (jana). Katika mashauri hayo ambayo hayakupata kuzungumzwa ndani ya miaka saba, mkurugenzi alitamka mbele ya Jaji kuwa jamhuri haina nia ya kuendelea tena na mashauri hayo,” imesema taarifa ya Mkondo.

Masheikh walioachwa huru ni pamoja na Sheikh Juma Yasin, Ustadhi Abdalla Juma Omar, Nassoro Said Amoor, Ali Nassoro Swala, Juma Zuberi Kitambi, Rajabu Ali Magomba, Hussein Mustafa Juma na Haruna Issa Nkuye.

Wengine ni, Buheti Yusuf Buheti, Seif Shaha Jongo, Yusuf Issa Rajab, Hassan Bakari Mnele, Ramia Shaaban Swaleh, Abdul Majid Juma Ludima na Rashid Hassan Mitambo.

Hatua hiyo ni muendelezo wa DPP Mwakitalu kufuta kesi za ugaidi zilizokuwa zinawakabili masheikh waliosota rumande kwa zaidi ya miaka mitano, ambapo hivi karibuni aliwafutia mashtaka masheikh 40.

Masheikh hao 40 walikuwa wanakabiliwa na mashtaka ya ugaidi katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kibaha.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB yang’ara maonesho OSHA

Spread the loveBenki ya NMB imebeba tuzo ya kampuni bora kwenye sekta...

Habari MchanganyikoKimataifa

Ruto amteua Kahariri kuwa mkuu wa majeshi

Spread the loveRAIS wa Kenya, William Ruto, amemteua Jenerali Charles Muriu Kahariri,...

Habari Mchanganyiko

Chongolo aonya viongozi vijiji kutouza NIDA kwa wageni

Spread the loveMKUU wa Mkoa wa Songwe, Daniel Chongolo amewaonya viongozi wa...

Habari Mchanganyiko

TUCTA, OSHA wataka kampuni za madini kuiga ubunifu wa GGML

Spread the loveSHIRIKISHO la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA) pamoja na Wakala...

error: Content is protected !!