Monday , 13 May 2024
Home Kitengo Maisha Afya Tanga kujenga Kituo cha Mifupa
Afya

Tanga kujenga Kituo cha Mifupa

Spread the love

 

MKUU wa Mkoa wa Tanga, Adam Malima amesema mkoa wake unakusudia kuanzisha kituo cha Mifupa (Orthopaedic Centre) kwa ajili ya watu wanaopata ajali katika Barabara ya Mkata-Handeni na wakazi wa Tanga kwa ujumla. Anaripoti Mwandishi Wetu, Tanga … (endelea).

Malima amesema hayo wilayani Handeni leo tarehe 27 Februari, 2022 alipokuwa akikagua maendeleo ya mradi wa ujenzi wa Hospitali ya Halmashauri ya Wilaya ya hiyo jana.

“Hii ndiyo njia kubwa baada ya hapa watu wanaopata ajali Dar es Salaam kituo cha kwanza labda ukatibiwe Tumbi (Kibaha mkoani Pwani), lakini ukishavuka Chalinze pale hakuna kituo kingine hadi unafika Tanga zaidi ya KCMC.

“Kwa hiyo tunataka hapa katikati tuwe na kituo cha kusaidia wanaopata ajali ambayo ni dharura. Kwa hiyo tumekubaliana, tumejenga hoja Wizara ya Afya imetusikia, Tamisemi (Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa) imetusikia kwa hiyo tujenge kituo pekee kitakachokuwa baina ya Tumbi na KCMC.

Lakini wakati tunazungumzia kituo hicho hili jengo lilitakiwa liwe limekwisha sasa tutakuwa tunafanya kama ulafi fulani maana unakuwa kama unaomba chakula kingine wakati ulichokuwa nacho hakijaisha huo ni ulafi,” amesema.

Malima amesema kukamilika kwa hospitali hiyo kutaamua hatima ya kituo hicho cha mifupa kwani nia ya kuwa nacho ni kubwa kutokana na umuhimu wake.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

AfyaHabari Mchanganyiko

Vituo 13 vyasitishiwa mkataba madai kutaka kupiga bilioni 4 za NHIF

Spread the loveVITUO vya kutoa huduma za afya 13, vimesitishiwa mikataba ya...

AfyaHabari za Siasa

Wizara afya kutumia Sh. 1.31 trilioni, huduma za kibingwa zapewa kipaumbele

Spread the loveWIZARA ya Afya, imeliomba Bunge lipitishe makadirio yake ya mapato...

AfyaHabari za Siasa

Vifo vitokanavyo na UKIMWI vyapungua

Spread the loveVIFO vinavyosababishwa na Upungufu wa Kinga Mwilini (UKIMWI), vimepungua kutoka...

AfyaHabari MchanganyikoHabari za Siasa

NBC yazindua kadi uanachama msalaba mwekundu

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

error: Content is protected !!