Thursday , 2 May 2024
Home Kitengo Michezo Yanga yajikita kileleni, yaibamiza Mtibwa Manungu
Michezo

Yanga yajikita kileleni, yaibamiza Mtibwa Manungu

Spread the love

 

KLABU ya Soka ya Yanga imeendelea kujichimbia kileleni mara baada ya kuibuka na alama tatu kwenye mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara dhidi ya Mtibwa. Anaripoti Kelvin Mwaipungu…(endelea)

Mchezo huo wa Ligi Kuu Tanzania Bara, ulipigwa hii leo Jumatano Tarehe 23 Februari 2022, kwenye dimba la Manungu Complex na Yanga kufanikiwa kuondoka na ushindi wa mabao 2-0.

Mabao ya Yanga kwenye mchezo huo yaliwekwa kambani na Sadio Ntibanzokiza kwenye dakika ya 45+5, mara baada ya mlinzi wa Mtibwa Sugar kufanya makosa, na Yanga kutumia nafasi hiyo na kufanya bao hilo kudumu mpaka mapumziko.

Kipindi cha pili kiliporejea, Yanga waliendelea kushambulia na kupelekea kuandika bao la pili kwenye dakika ya 65, likiwekwa kambani na Fiston Mayele.

Bao hilo limekuwa la saba kwa mshambuliaji huyo, toka ajiunge na timu hiyo kwenye dirisha kubwa la usajili mwezi Agosti, akitokea klabu ya AS Vita ya nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Yanga.

Mayele kwa sasa anashika nafasi ya pili katika upachikaji mabao wa Ligi Kuu Tanzania Bara, sawa na George Mpole, ambaye naye amepachika mabao saba mpaka sasa, huku kinara kwenye chati hiyo akiwa Ralient Lusajo wa Namungo FC, ambaye amepachika mabao 10 mpaka sasa.

Kwa ushindi huo Yanga inafikisha jumla ya alama 39, point inane nyuma ya Simba waliokuwa kwenye nafasi ya pili huku wote wakiwa na michezo 15.

Mchezo unakuja Yanga itakuwa nyumbani, kuwakalibisha Kagera Sugar, mchezo utakaopigwa Jumapili ya Tarehe 27 Februari 2022, kwenye dimba la Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam majira ya saa 1 usiku.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoMichezo

Wanamichezo Mei Mosi wachangia wahitaji vitu vya mil. 11.5

Spread the loveWanamichezo wanaoshiriki Michezo ya Mei Mosi Taifa 2024 jijini Arusha...

Michezo

Usiku wa Ulaya umerejea kibabe kabisa

Spread the love  LIGI ya Mabingwa barani Ulaya imerejea tena na awamu...

Habari MchanganyikoMichezo

Mambo ya Ndani, Ulinzi zang’ara michezo ya Mei Mosi Arusha

Spread the loveRais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi nchini (TUCTA), Tumaini...

Michezo

Beti na Meridianbet mechi za leo

Spread the love IKIWA leo hii ni Jumapili tulivu kabisa, Meridianbet wanamkwambia...

error: Content is protected !!