Friday , 3 May 2024
Home Kitengo Michezo Shabiki Simba ajinyonga, siku ya mchezo dhidi ya Mbeya city
Michezo

Shabiki Simba ajinyonga, siku ya mchezo dhidi ya Mbeya city

Spread the love

 

SHABIKI wa klabu ya Simba Khalfan Mwambena mwenye umri wa miaka 17, mkazi wa kata ya Kholobe mkoani Mbeya amekutwa amejinyonga muda mchache kabla ya kuanza kwa mchezo kati ya Simba na Mbeya City. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea)

Kupitia taarifa iliyotolewa na uongozi wa klabu ya Simba hii leo, Tarehe 19 Januari 2021 ilieleza kuwa kaimu kamanda wa polisi mkoa wa Mbeya Christina Musyani alithibitisha kuwa marehe alijinyonga kabla ya mchezo huo na si baada ya mchezo huo kama watu wengi wanavyoripoti.

Mchezo huo wa Ligi Kuu Tanzania Bara ulipigwa kwenye dimba la sokoine tarehe 17 Januari, 2021 ambapo Simba alipoteza kwa bao 1-0, bao la dakika 19 lililofungwa na Paul Nonga.

Taarifa ya klabu ya Simba iliyomnukuu kamanda Musyani iliendelea kueleza kuwa, marehemu aliacha ujumbe kwenye karatasi uliosemeka kuwa “ Naipenda sana Simba na nikifa nizikwe na jezi ya Simba”

Licha ya kupoteza mchezo huo Simba imeendelea kusalia kwenye nafasi ya pili, wakiwa na pointi zao 24 pointi nane nyuma ya Yanga wenye alama 32 ambao wapo kwenye kilele cha msimamo huo.

Simba imepoteza mchezo huo wa kwanza wa Ligi Kuu Tanzania Bara, toka kuanza kwa msimu mpya wa 2021/22 mara baada ya kucheza dakika 919, sawa na michezo 11.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Europa na Conference kukupatia pesa ndefu leo

Spread the love  ALHAMISI ya leo tutaenda kushuhudia mitanange ya kukata na...

Habari MchanganyikoMichezo

Wanamichezo Mei Mosi wachangia wahitaji vitu vya mil. 11.5

Spread the loveWanamichezo wanaoshiriki Michezo ya Mei Mosi Taifa 2024 jijini Arusha...

Michezo

Usiku wa Ulaya umerejea kibabe kabisa

Spread the love  LIGI ya Mabingwa barani Ulaya imerejea tena na awamu...

Habari MchanganyikoMichezo

Mambo ya Ndani, Ulinzi zang’ara michezo ya Mei Mosi Arusha

Spread the loveRais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi nchini (TUCTA), Tumaini...

error: Content is protected !!