Friday , 3 May 2024
Home Kitengo Michezo Chama arejea Simba, atangazwa rasmi
MichezoTangulizi

Chama arejea Simba, atangazwa rasmi

Clatous Chama
Spread the love

 

KLABU ya soka ya Simba imetangaza rasmi kumrejesha kiungo wake raia wa Zambia Clatous Chama, mara baada ya kufanikiwa kumsajili tena akitokea kwenye klabu ya RS Berkane ambapo alivunja mkataba nao ara baada ya kudumu kwa miezi mitano. Anaripori Kelvin Mwaipungu…(endelea)

Chama amerejea tena Simba kwa kusaini mkataba wa miaka miwili utakaomfanya adumu kwenye klabu hiyo hadi msimu wa 2021/22.

Mchezaji huyo amejiunga tena na Simba kwenye dirisha dogo la usajili akitokea RS Berkane inayoshiriki Ligi Kuu nchini Morocco kufuatia kutopata nafasi ya kutosha ya kucheza kwenye kikosi cha kwanza chini ya kocha Frolence Ibenge kutoka Jamhuri ya Demokrasia ya Congo toka alip[ojiunga nayo kwenye dirisha kubwa mwezi Agosti, 2021.

Uongozi wa Simba ulimfuatilia muda mrefu mchezaji huyo ambaye alihitaji mwenyewe kuvunja mkataba huo na kurejea nchini kwenye kikosi cha mabingwa watetezi wa Ligi Kuu Tanzania Bara ambapo alicheza kwa mafanikio.

Mchezaji huyo anakuja ndani ya klabu ya Simba kuchukua nafasi ya Duncan Nyoni ambaye klabu ya Simba imevunja mkataba nae kufuatia kutoonyesha kiwango kizuri miezi michache toka ajiunge na klabu hiyo.

Ikumbukwe Chama alifika nchini kwenye msimu wa 2018/19 na kucheza kwa mafanikio makubwa ndani ya klabu ya Simba akitokea nchini Zambia kwenye klabu ya Lusaka Dynamos.

Katika kipindi cha miaka mitatu Chama amefanikiwa kuipa Simba ubingwa wa Ligi Kuu Tanzania Bara mara tatu, Ubingwa wa kombe la Shirikisho mara mbili na kuifikisha hatua ya robo fainali ya Ligi ya Mabingwa Afrika mara mbili.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Sabaya afutiwa kesi, ruksa kugombea uongozi

Spread the loveMwendesha Mashtaka Mkuu wa Serikali DPP leo Ijumaa amefuta rufaa...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema kwafukuta kisa chaguzi, Lissu aibua tuhuma nzito

Spread the loveCHAGUZI za kusaka viongozi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo...

Habari MchanganyikoTangulizi

Kimbunga “HIDAYA” chaendelea kuimarika, wananchi wapewa tahadhari

Spread the loveMAMLAKA ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) inaendelea kutoa taarifa...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema kumshtaki Rais Samia

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimetishia kumfungulia kesi ya...

error: Content is protected !!