Sunday , 19 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa 9 wajitosa CCM kumrithi Ndugai
Habari za SiasaTangulizi

9 wajitosa CCM kumrithi Ndugai

Spread the love

 

WANACHAMA tisa wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) nchini Tanzania wamejitosa kuchukua fomu kuwania uspika wa Bunge la nchi hiyo. Anaripoti Danson Kaijage, Dodoma…(endelea).

Fomu hizo zimeanza kutolea leo Jumatatu, tarehe 10-15 Januari 2022, katika Ofisi ndogo za Lumumba jijini Dar es Salaam, Kisiwandui, Zanzibar pamoja na Makao Makuu ya chama hicho, jijini Dodoma.

CCM inaendesha mchakato wa kumpata mgombea uspika, baada ya aliyekuwa spika wa Bunge, Job Ndugai kujiuzulu nafasi yake tarehe 6 Januari 2022, kutokana na kauli yake aliyoitoa kuhusu serikali kukopa kuibua mjadala mkali.

Akitoa taarifa ya uchukuaji fomu, katibu msaidizi mkuu idara ya oganaizesheni, Salomon Itunda amesema, waliochukulia ofisi ya Dodoma ni sita na Lumumba jijini Dar es Salaam wakiwa watatu.

Kati ya wanachama hao tisa waliojitosa kuchukua fomu yumo, Naibu Spika wa Bunge, Dk. Tulia Ackson pamoja na Mbunge wa Mlimba mkoani Morogoro, Godwin Kunambi waliochukua fomu zao jijini Dodoma.

Wengine waliochukua Dodoma ni, Dk. Saimon Ngatunga, Tumsifu Mwansamale,
Merkion Ndofu na Ambwene Kajula.

Waliochukulia ofisi ya Lumumba ni, Patrick Nkandi, Hamidu Chamani na Stephen Massele ambaye aliwahi kuwa mbunge wa Shinyanga Mjini na Makamu wa Kwanza wa Rais wa Bunge la Afrika (PAP).

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za SiasaTangulizi

Wakili Mwabukusi anusurika kufungiwa, asema hatarudi nyuma

Spread the loveWAKILI Boniface Mwabukusi amesema kuwa hatorudi nyuma kuwatetea Watanzania na...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

RC Chongolo atangaza ‘vita’ kwa wanaovusha wageni kinyemela

Spread the loveKATIKA kulinda usalama wa nchi kupitia mpaka wa Songwe, Mkuu...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

RUWASA yachongewa, yateketeza mamilioni kwa maji yenye magadi

Spread the loveSAKATA la ukosefu wa maji wilayani Momba mkoani Songwe limezidi...

Habari MchanganyikoHabari za SiasaTangulizi

Lissu akabidhiwa gari lake, aomba msaada wa matengenezo

Spread the loveMakamu Mwenyekiti wa Chadema Bara, Tundu Lissu leo Ijumaa amekabidhiwa...

error: Content is protected !!