Thursday , 2 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Hukumu kesi ya Membe, Musiba yapigwa kalenda
Habari Mchanganyiko

Hukumu kesi ya Membe, Musiba yapigwa kalenda

Cyprian Musiba
Spread the love

 

HUKUMU ya kesi ya madai ya kashfa iliyofunguliwa na aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Nje katika Serikali ya Awamu ya Nne, Bernard Membe dhidi ya mwanahabari anayejitambulisha mwanaharakati huru, Cyprian Musiba imepigwa kalenda hadi Oktoba 28, 2021. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Katika kesi hiyo namba 220 ya mwaka 2018, Membe amemshtaki Musiba, Mhariri wa gazeti la Tanzanite na Wachapishaji wa gazeti hilo ambapo anawadai Tsh. Bilioni 10 kwa kumchafua.

Hukumu ya kesi hiyo iliyokuwa itolewe leo Jumanne tarehe 12 Oktoba, 2021 na Jaji Joaquine De Mello imeahirishwa kwa sababu haijakamilika kuandikwa.

Wakili wa Membe, Jonathan Mndeme amesema hukumu hiyo imeahirishwa hadi Oktoba 28 kwa kuwa Jaji De Mello bado hajamaliza kuiandika.

Bernard Membe

Mbali na Musiba, wadaiwa wengine katika kesi hiyo ni Mhariri wa Gazeti la Tanzanite linalomilikiwa na Musiba na kampuni ya Tz Information and Media Consultant Ltd.

Musiba na wenzake katika kesi hiyo anashtakiwa kwa kumtuhumu Membe kuwa anamhujumu Rais John Magufuli asitekeleze majukumu yake ya kuwaletea wananchi maendeleo huku akidai kwamba mbinu mojawapo ya kukamilisha hujuma hizo ni maandalizi anayofanya kugombea urais mwaka 2020 kupitia CCM.

Bernard Membe alikuwa miongoni mwa wagombea Urais katika Uchaguzi Mkuu 2015.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

Equity Bank yaendelea kusotea mabilioni ya fedha mahakama rufani

Spread the loveBENKI za Equity ya Tanzania na Kenya, zimeendelea kupambana mahakamani...

Habari Mchanganyiko

NEMC yatoa elimu matumizi sahihi ya zebaki kwa wachimbaji

Spread the loveBARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC)...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Oryx gesi yagawa mitungi, majiko 100 kwa waandishi wa habari Dar

Spread the loveKAMPUNI ya Oryx Gesi Tanzania imegawa mitungi 100 ya gesi...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

error: Content is protected !!