Friday , 3 May 2024
Home Kitengo Michezo Alichoandika Mo Dewji kifo cha Hanspope
Michezo

Alichoandika Mo Dewji kifo cha Hanspope

Spread the love

 

MWENYEKITI wa Bodi ya Wakurugenzi wa Klabu ya Simba ya Dar es Salaam nchini Tanzania, Mohamed Dewji “Mo Dewji” amesema ni vigumu kukubali kwamba Zakaria Hans Pope amefariki dunia. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Hans Pope, aliyekuwa mjumbe wa bodi ya Simba na mwenyekiti wa kamati ya usajili wa timu hiyo, alifarini dunia usiku wa jana Ijumaa tarehe 10 Septemba 2021, katika Hospitali ya Agha Khan jijini Dar es Salaam alipokuwa akipatiwa matibabu.

Dewji ambaye pia ni mwekezaji ndani ya mabingwa hao mara nne mfululizo wa ligi kuu Tanzania Bara, ameweka picha aliyopita yeye na Hans Pope huku akisema;

“Moyo wangu una maumivu makali sana. Bado ni vigumu kukubali kwamba Mjumbe wetu wa bodi Zakaria Hans Poppe hatunaye tena.

Pole kwa familia, ndugu, jamaa, marafiki na Wanasimba kwa ujumla kwa msiba huu mzito. Mwenyezi Mungu aipumzishe roho yake mahali pema peponi.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Europa na Conference kukupatia pesa ndefu leo

Spread the love  ALHAMISI ya leo tutaenda kushuhudia mitanange ya kukata na...

Habari MchanganyikoMichezo

Wanamichezo Mei Mosi wachangia wahitaji vitu vya mil. 11.5

Spread the loveWanamichezo wanaoshiriki Michezo ya Mei Mosi Taifa 2024 jijini Arusha...

Michezo

Usiku wa Ulaya umerejea kibabe kabisa

Spread the love  LIGI ya Mabingwa barani Ulaya imerejea tena na awamu...

Habari MchanganyikoMichezo

Mambo ya Ndani, Ulinzi zang’ara michezo ya Mei Mosi Arusha

Spread the loveRais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi nchini (TUCTA), Tumaini...

error: Content is protected !!