MWENYEKITI wa Bodi ya Wakurugenzi wa Klabu ya Simba ya Dar es Salaam nchini Tanzania, Mohamed Dewji “Mo Dewji” amesema ni vigumu kukubali kwamba Zakaria Hans Pope amefariki dunia. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).
Hans Pope, aliyekuwa mjumbe wa bodi ya Simba na mwenyekiti wa kamati ya usajili wa timu hiyo, alifarini dunia usiku wa jana Ijumaa tarehe 10 Septemba 2021, katika Hospitali ya Agha Khan jijini Dar es Salaam alipokuwa akipatiwa matibabu.
Dewji ambaye pia ni mwekezaji ndani ya mabingwa hao mara nne mfululizo wa ligi kuu Tanzania Bara, ameweka picha aliyopita yeye na Hans Pope huku akisema;
Kaka yangu, Zakaria Hans Poppe, nimefanya kazi na wewe kwa miaka mingi, na kila siku uliweka maslahi ya Simba mbele. Kaka yangu ulikua na wema wa kipekee, na ulikua wa kwanza na ulinyooka linapokuja suala la kuilinda Simba, hukuwa na maslahi binafsi.
Nitakukumbuka sana 🙏🏾
— Mohammed Dewji MO (@moodewji) September 11, 2021
“Moyo wangu una maumivu makali sana. Bado ni vigumu kukubali kwamba Mjumbe wetu wa bodi Zakaria Hans Poppe hatunaye tena.
Pole kwa familia, ndugu, jamaa, marafiki na Wanasimba kwa ujumla kwa msiba huu mzito. Mwenyezi Mungu aipumzishe roho yake mahali pema peponi.”
Leave a comment