Friday , 3 May 2024
Home Kitengo Michezo Dk. Abbas aitaka Cosota kuwabana ‘wanaomnyonya’ Mb Dogg
Michezo

Dk. Abbas aitaka Cosota kuwabana ‘wanaomnyonya’ Mb Dogg

Spread the love

 

WIZARA ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo nchini Tanzania, imeiagiza Taasisi ya Hakimiliki nchini humo (COSOTA), kufuatilia na kuhakikisha msanii Mb Dogg anapata haki zake kutoka kampuni ambazo zimetumia kazi zake bila yeye kupata chochote. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Agizo hilo, limetolewa jana Alhamisi tarehe 22 Julai 2021, jijini Dar es Salaam na Katibu Mkuu wa wizara hiyo, Dk. Hassan Abbasi, alipomwita msanii huyo aliyekuwa amelalamika kwenye mitandao ya kijamii akiomba msaada wa kupiganiwa haki zake.

“Hili limeisha, COSOTA simamieni msanii huyu apate haki zake kutoka kampuni za ZIIKI na kampuni nyingine iitwayo ZEZE ambayo iko Kenya,” alisema Dk. Abbas na kuongeza:

“Mtawasiliana mara moja na wenzetu wa Kenya kuhakikisha kazi za Mb Dogg zinapata stahiki yake.”

Dk. Abbasi pia ameitaka COSOTA kuendelea kuweka kanuni zinazowalinda wasanii wa nchini huku akisisitiza uwazi katika makampuni yanayouza kazi za muziki

Kwa upande wake, Mb Dogg alisema, amekuwa katika juhudi za kurejea kimuziki lakini alishangazwa na kubaini kuwa nyimbo zake nyingi zinatumika katika mitandao ya kuuza muziki bila aidha makubaliano au pale penye makubaliano bila kupewa stahiki zake.

Pia, ameishukuru Serikali kwa kuingilia kati swala hilo na anaamini kupitia Serikali kwa sasa anaweza kupata haki yake.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Ligi mbalimbali za pesa kuendelea leo

Spread the love Ijumaa ya leo ambapo mechi mbalimbali zinaendelea Duniani Meridianbet...

Michezo

Europa na Conference kukupatia pesa ndefu leo

Spread the love  ALHAMISI ya leo tutaenda kushuhudia mitanange ya kukata na...

Habari MchanganyikoMichezo

Wanamichezo Mei Mosi wachangia wahitaji vitu vya mil. 11.5

Spread the loveWanamichezo wanaoshiriki Michezo ya Mei Mosi Taifa 2024 jijini Arusha...

Michezo

Usiku wa Ulaya umerejea kibabe kabisa

Spread the love  LIGI ya Mabingwa barani Ulaya imerejea tena na awamu...

error: Content is protected !!