Thursday , 25 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Magaidi 30 wauawa Msumbiji
Kimataifa

Magaidi 30 wauawa Msumbiji

Spread the love

 

WANAJESHI wa Rwanda, walioko nchini Msumbiji kukabiliana na ugaidi, wamewauwa wanamgambo wa kiislamu 30, waliovamia Jimbo la Cabo Delgado, Kaskazini mwa nchi hiyo. Inaripoti BBC … (endelea).

Taarifa hiyo imetolewa hivi karibuni na mamlaka za usalama nchini Msumbiji.

Mamlama hizo zimesema kuwa, wanamgambo hao wa kiislamu wanaoshukiwa kuwa na uhusiano na kundi la Al Shabab, waliuawa katika doria zilizofanywa na Wanajeshi wa Rwanda, katika msitu ulioko karibu na mji wa bandari ya Palma.

Serikali ya Rwanda mwanzoni mwa mwezi huu, ilituma wanajeshi wake 1,000 kwa ajili ya kukabiliana na magaidi hao, wanaoisumbua Msumbiji zaidi ya miaka minne.

Pia, nchi ya Ureno na Jumuiya za Kusini mwa Afrika, zimepeleka wanajeshi kwa ajili ya kukabiliana na wanamgambo hao. Ikiwa pamoja na kutoa mafunzo kwa wanajeshi wa Msumbiji.

Wanamgambo hao wamewauwa maelfu ya watu, huku watu zaidi ya laki nane, wakikimbia makazi yao.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

Habari MchanganyikoKimataifa

Tetemeko la ardhi laua 7, lajeruhi 800 Taiwan

Spread the loveWatu wapatao saba wamefariki dunia na wengine zaidi ya 800...

error: Content is protected !!