Thursday , 28 March 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Uchunguzi Covid-19: China yaigomea WHO
Kimataifa

Uchunguzi Covid-19: China yaigomea WHO

Naibu Waziri wa Afya wa China, Zeng Yixin
Spread the love

 

SERIKALI ya China, imepinga mpango wa Shirika la Afya Duniani (WHO), wa kurudia uchunguzi dhidi ya mlipuko wa kwanza wa Virusi vya Corona. Inaripoti BBC … (endelea).

Katika mpango wake huo, WHO inataka kukagua maabara ambazo virusi hivyo viligundulika kwa mara , Desemba 2019, zilizopo kwenye Jiji la Wuhan nchini humo.

Akizungumza na wanahabari jana tarehe 23 Julai 2021, Naibu Waziri wa Afya wa China, Zeng Yixin, alisema hawatakubali uchunguzi huo, kwa madai kwamba unakiuka itifaki za maabara za nchi hiyo.

“Tunatumaini kwamba WHO itapitia kwa uzito mapitio na maoni yaliyotolewa na wataalamu wa China. Na kulichukulia janga hili kama suala la kisayansi na kuondoa uingiliaji wa kisiasa,” alisema Zeng.

Watalaamu wa WHO walitembelea Jiji la Wuhan nchini China, Januari 2021, kwa ajili ya kufanya uchunguzi katika maabara zinazoshukiwa kuzalisha virusi hivyo.

Mkuu wa WHO, Dk. Tedros Adhanom Ghebreyesus

Mkuu wa WHO, Dk. Tedros Adhanom Ghebreyesus, aliiomba Serikali ya China itoe ushirikiano katika uchunguzi huo, ambao ungehusisha taasisi za utafiti wa kisayansi.

Dk. Tedros aliitaka China iwe wazi na kushirikiana na wachunguzi wa WHO, ikiwemo kutoa data za wagonjwa ambazo hazijashirikishwa katika uchunguzi wa kwanza uliofanywa na shirika hilo.

Tangu mlipuko wa virusi hivyo utokee mwishoni mwa 2019 na kusababisha ugonjwa wa homa kali ya mapafu (Covid-19), umeuwa watu takribani milioni nne duniani.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifa

Mwanaye rais jela miaka miaka 6 kwa dawa za kulevya

Spread the loveMwanawe rais wa zamani wa Guinea-Bissau amehukumiwa kifungo cha miaka...

Habari za SiasaKimataifa

Faye aahidi kuongoza kwa unyenyekevu, wagombea wenzie wakubali yaishe

Spread the loveMgombea wa upinzani Senegal, Bassirou Diomaye Faye anajiandaa kuwa rais...

Habari MchanganyikoKimataifa

Wanafunzi 130 waliokuwa wametekwa nyara waokolewa

Spread the loveZaidi ya wanafunzi 130 wa shule ya msingi LEA na...

Habari MchanganyikoKimataifa

Mgombea upinzani aongoza uchaguzi wa Rais Senegal

Spread the loveMgombea wa upinzani nchini Senegal, Bassirou Diomaye Faye ameonekana kuongoza...

error: Content is protected !!