Thursday , 2 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Lissu atua Kenya kuzindua kitabu chake
Habari za SiasaTangulizi

Lissu atua Kenya kuzindua kitabu chake

Tundu Lissu, Makamu Mwenyekiti Chadema
Spread the love

 

TUNDU Lissu, Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Demokrais na Maendeleo (Chadema), yupo nchini Kenya kwa maandalizi ya uzinduzi wa kitabu chake. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).

Kwa mujibu wa mwanasheria wake, Profesa George Wajackoya wakati akizungumza na mtandao wa Nation Africa leo tarehe 24 Juni 2021, Lissu atazindua kitabu chake ‘Vivuli- Bunge na Uwajibikaji kwa Afrika Mashariki’ Ijumaa tarehe 25 Juni 2021.

Prof. Wajackoya amesema “ni kweli (Lissu) yupo nchini (Kenya) kwa ajili ya kuzindua kitabu chake katika Hoteli ya Windsor.”

Lissu ametua Kenya akitokea Ubelgiji alikokwenda baada ya uchaguzi mkuu 2020. Kwenye uchaguzi huo, alikuwa mgombea urais Tanzania Bara kupitia Chadema.

Awali, Lissu alikwenda Ubelgiji kwa matibabu baada ya kushambuliwa kwa risasi jijini Dodoma mwaka 2017, kutokana na shambulizi hilo, amefanyiwa operesheni mara 25.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari za Siasa

Mavunde aomba bilioni 231.9 bajeti wizara ya madini

Spread the loveWAZIRI wa Madini, Anthony Mavunde leo Jumanne amewasilisha hotuba ya...

Habari za SiasaTangulizi

Lissu amjibu Fatma Karume kuhusu Rais Samia

Spread the love  MAKAMU Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)...

Habari za SiasaTangulizi

Dk. Slaa: Watanzania iungeni mkono Chadema uchaguzi 2025

Spread the loveMWANASIASA mkongwe nchini Tanzania, Dk. Wilbroad Slaa, amewataka watanzania wakiunge...

error: Content is protected !!