Friday , 19 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Lissu atua Kenya kuzindua kitabu chake
Habari za SiasaTangulizi

Lissu atua Kenya kuzindua kitabu chake

Tundu Lissu, Makamu Mwenyekiti Chadema
Spread the love

 

TUNDU Lissu, Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Demokrais na Maendeleo (Chadema), yupo nchini Kenya kwa maandalizi ya uzinduzi wa kitabu chake. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).

Kwa mujibu wa mwanasheria wake, Profesa George Wajackoya wakati akizungumza na mtandao wa Nation Africa leo tarehe 24 Juni 2021, Lissu atazindua kitabu chake ‘Vivuli- Bunge na Uwajibikaji kwa Afrika Mashariki’ Ijumaa tarehe 25 Juni 2021.

Prof. Wajackoya amesema “ni kweli (Lissu) yupo nchini (Kenya) kwa ajili ya kuzindua kitabu chake katika Hoteli ya Windsor.”

Lissu ametua Kenya akitokea Ubelgiji alikokwenda baada ya uchaguzi mkuu 2020. Kwenye uchaguzi huo, alikuwa mgombea urais Tanzania Bara kupitia Chadema.

Awali, Lissu alikwenda Ubelgiji kwa matibabu baada ya kushambuliwa kwa risasi jijini Dodoma mwaka 2017, kutokana na shambulizi hilo, amefanyiwa operesheni mara 25.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Habari za SiasaTangulizi

Tanzania, Uturuki zanuia kukuza biashara, uwekezaji

Spread the loveSERIKALI za Tanzania na Uturuki zimekubaliana kuendeleza dhamira ya kuimarisha...

Habari za Siasa

Tume huru ya uchaguzi yatangaza ajira watendaji daftari wapiga kura

Spread the love  TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC), imetangaza nafasi...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema yatangaza ruti awamu ya pili maandamano

Spread the love  CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimesema awamu ya...

error: Content is protected !!