Wednesday , 22 May 2024
Home Kitengo Maisha Afya Tanzania kuajiri wataalamu bingwa wa moyo 12 kutoka nje
AfyaHabari za Siasa

Tanzania kuajiri wataalamu bingwa wa moyo 12 kutoka nje

Spread the love

 

RAIS wa Tanzania, Samia Suluhu hassan, amesema atalifanyia kazi ombi la Taasisi ya Moyo ya jakaya Kikwete (JKCI), la kuajiri watalaam 12 wa magonjwa ya moyo, kutoka nje ya nchi. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea).

Rais Samia amesema hayo leo Jumamosi, tarehe 12 Juni 2021, akizindua mitambo miwili ya kisasa ya uchunguzi na tiba ya moyo ya JKCI, iliyosimikwa kwa Sh.4.6 bilioni.

“Kuhusu ombi la kibali cha ajira za wataalamu 12 kutoka nje, ikiwemo wanaofanya kazi za madaktari bingwa watatu, tumepokea maombi yote tutayafanyia kazi,” amesema Rais Samia.

Ombi hilo lilitolewa na Mkurugenzi Mtendaji wa JKCI, Prof. Mohammed Janabi, akielezea changamoto za utendaji wa taasisi hiyo, ikiwemo uhaba wa watalaamu.

Pia, Prof. Janabi alimuomba Rais Samia atoe Sh.2 bilioni, kwa ajili ya kuchangia ujenzi wa jengo jipya la taasisi hiyo, unaogharimu Sh.4 bilioni.

Kuhusu ombi la fedha hizo, Rais Samia amesema Serikali yake itatoa fedha hizo.

“Mkurugenzi amewasilisha ombi la fedha za ujenzi wa jengo jipya la taasisi linalogharimu Sh.4 bilioni, nataka nimhakikishie kwamba Sh.2 bilioni za Serikali zitapatikana,” amesema Rais Samia.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

AfyaKimataifaTangulizi

Waliowekewa damu yenye VVU, homa ya ini kulipwa fidia trilioni 32.9

Spread the loveWaziri mkuu wa Uingereza, Rishi Sunak ameahidi kulipa fidia ya...

Habari za SiasaTangulizi

Serikali yanawa mikono fidia Kimara-Kibamba

Spread the loveSERIKALI imewataka waathiriwa wa bomoabomoa ya upanuzi wa barabara ya...

Habari za Siasa

Watumishi 25,039, taasisi 65 wahamia Dodoma

Spread the loveSerikali imesema hadi sasa, jumla ya watumishi 25,039 kutoka Serikali...

Habari za SiasaKimataifa

Balozi Kasike ateta na mjumbe wa FRELIMO

Spread the loveBalozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Msumbiji, Phaustine...

error: Content is protected !!