Saturday , 4 May 2024
Home Kitengo Michezo Mkude apiga simu Yanga 
Michezo

Mkude apiga simu Yanga 

Spread the love

 

MARA baada ya kuripotiwa kuwa na matatizo ya kinidhamu na klabu yake wakati walipokuwa kwenye mchezo wa Ligi ya Mabingwa nchini Afrika Kusini dhidi ya Kaizer Chiefs kiungo wa klabu ya Simba, Jonas Mkude ameonekana kupindukia upande wa pili wa wapinzani wao klabu ya Yanga kufanya mawasiliano na moja ya kiongozi. Anaripoti Kelvin Mwaipungu…(endelea)

Mkude kwa sasa shauri lake juu ya utovu wa nidhamu limefikishwa kwenye kamati ya nidhamu ya klabu hiyo chini ya mwenyekiti wake Suleiman Kova na kutolewa maamuzi hivi karibuni.

Mtoaji taarifa aliliambia Raia Mwema, kwamba mchezaji huyo alifanya mawasiliano zaidi ya mara tatu na kiungozi wa juu mwandamizi wa klabu ya Yanga na kudai kuwa kama mambo yataenda kombo kwenye klabu yake ya sasa ya Simba yupo tayari kukipiga ndani ya Jangwani.

“Mkude mwenyewe alimpigia simu kiongozi huyo zaidi ya mara tatu na aliongea naye kwa muda mrefu na kumwambia yupo tayari kucheza Yanga kama Simba wakimzingua,” kilisema chanzo hiko.

Aidha chanzo hiko kilendelea kueleza kuwa, kilichobaki kwa sasa mchezaji huyo kusubiri maamuzi ya kamati ya maadili dhidi yake na kuna mpango wa kmshusha timu ya vijana kama sehemu ya adhabu kwa kufanya kosa hilo kwa mara ya pili.

Je ni maamuzi gani ambayo mchezaji huyo atayachukua mara baada ya sakata hilo? soma gazeti lako la Raia Mwema la leo kwa habari zaidi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Ligi mbalimbali za pesa kuendelea leo

Spread the love Ijumaa ya leo ambapo mechi mbalimbali zinaendelea Duniani Meridianbet...

Michezo

Europa na Conference kukupatia pesa ndefu leo

Spread the love  ALHAMISI ya leo tutaenda kushuhudia mitanange ya kukata na...

Habari MchanganyikoMichezo

Wanamichezo Mei Mosi wachangia wahitaji vitu vya mil. 11.5

Spread the loveWanamichezo wanaoshiriki Michezo ya Mei Mosi Taifa 2024 jijini Arusha...

Michezo

Usiku wa Ulaya umerejea kibabe kabisa

Spread the love  LIGI ya Mabingwa barani Ulaya imerejea tena na awamu...

error: Content is protected !!