Thursday , 25 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Bundi atua kwa Makonda, Mnyeti
Habari Mchanganyiko

Bundi atua kwa Makonda, Mnyeti

Paul Makonda
Spread the love

 

BAADHI ya wadau wa haki za binadamu nchini Tanzania, wametaka serikali kukunjua makucha yake kwa kuanzisha uchunguzi maalum kwa watumishi wa umma, wanaotuhumiwa kwa matumizi mabaya ya madaraka. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).

Miongoni mwa wanaotajwa kuwa wanastahili kuchunguzwa, ni pamoja na aliyekuwa mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda; aliyekuwa mkuu wa mkoa wa Manyara, Alexander Mnyeti na mkuu wa wilaya ya Rorya, mkoani Mara, Simon Ezekiel Odunga.

Mnyeti na Makonda, wanatuhumiwa kwa matumizi mabaya ya madaraka, wakati wakiwa viongozi wa umma, katika kipindi cha utawala wa Hayati Rais John Pombe Magufuli.

Kabla ya kuwa mkuu wa mkoa wa Manyara, Mnyeti ambaye kwa sasa, ni mbunge wa Misungwi, mkoani Mwanza, alikuwa mkuu wa wilaya ya Arumeru, mkoani Arusha.

Alexander Mnyeti 

Makonda, aliondoka kwenye utumishi wa umma, tarehe 15 Julai 2020, baada ya uteuzi wake kufutwa na Hayati Rais Magufuli, kufuatia hatua yake ya kujitosa kwenye mbio za ubunge katika jimbo la Kigamboni.

Kwa nini Makonda, Mnyeti na Onduga wachunguzwe? Kipi wanatuhumiwa kukitenda? Soma Gazeti la Raia Mwema la leo Jumanne, tarehe 8 Juni 2021.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

THRDC yaongeza mkataba wa ushirikiano na ABA

Spread the love  MTANDAO wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC),...

error: Content is protected !!