Friday , 19 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Rais Samia atoa utaratibu mpya maiti kutokuzuiwa
Habari MchanganyikoTangulizi

Rais Samia atoa utaratibu mpya maiti kutokuzuiwa

Spread the love

 

RAIS wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, amemuagiza Waziri wa Afya, Dk. Dorothy Gwajima, aandae utaratibu mpya wa malipo ya madeni ya gharama za matibabu, za wagonjwa wanaofariki dunia, ili kuondoa changamoto ya maiti kuzuiwa hospitalini. Anaripoti Nasra Bakari, DMC…(endelea).

Rais Samia ametoa agizo hilo leo Jumanne, tarehe 8 Juni 2021, akizungumza na wanawake wa Mkoa wa Dodoma.

“Hili la kudaiwa wakati mgonjwa amefariki, waziri wekeni mpango mzuri. Ambapo kama mgonjwa amefariki, maiti yake itatolewa. Kweli kidini tunaambiwa mtu asiende kuzikwa mpaka deni liwe limelipwa, lakini si deni la Serikali,” amesema Rais Samia.

Kiongozi huyo wa Tanzania, ameitaka wizara hiyo kuweka utaratibu utakaowezesha ndugu na jamaa wanaofiwa, kulipa madeni ya gharama za matibabu, baada ya kumzika ndugu yao.

“Naomba muweke mpango mzuri na hapa nataka wananchi wanielewe, sio kwamba deni lisilipwe bali kuwekwe mpango mzuri wa kulipa deni bila kuzuia maiti,” amesema Rais Samia.

Aidha, Rais Samia ametoa wito kwa wananchi, kulipa gharama za matibabu wakati mgonjwa anaendelea kupata huduma hiyo, ili kuepuka mrundikano wa madeni, ambao hawataweza kulipa kwa wakati mmoja.

“Na mpango mzuri ni kutoa gharama za matibabu wakati matibabu yanaendelea, bila kusubiri siku ya mwisho mgonjwa amefariki, unamwambia milioni tatu huku ana maiti ya kusafirisha. Ana deni maiti hatoki bila kuilipa. Naomba muweke mpango mzuri kushughulikia hili,” amesema Rais Samia.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wauguzi, madaktari 1000 kugawiwa mitungi ya Oryx Gas

Spread the loveKAMPUNI ya Oryx Gas na Taasisi ya Doris Mollel Foundation...

Habari Mchanganyiko

Tanzania yachaguliwa Makamu wa Rais Tume ya Shirika la Hali ya Hewa Duniani

Spread the love  TANZANIA kupitia Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA)...

Habari Mchanganyiko

NEMC yaonya wanaojenga bila tathmini ya mazingira

Spread the loveBARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC),...

Habari za SiasaTangulizi

Mpina ataka Waziri Majaliwa ajiuzulu, akosoa teuzi za mawaziri

Spread the love  MBUNGE wa Kisesa, Luhaga Mpina, amemtaka Waziri Mkuu, Kassim...

error: Content is protected !!