Saturday , 18 May 2024
Home Kitengo Michezo Yanga yaigomea TFF, kuingiza timu saa 11 jioni
MichezoTangulizi

Yanga yaigomea TFF, kuingiza timu saa 11 jioni

Hassan Bumbuli, Afisa Habari na Mawasiliano wa Yanga
Spread the love

 

MABINGWA wa Kihistoria nchini Tanzania, Yanga ya jijini Dar es Salaam umesema, utaipeleka timu yao katika Uwanja wa Benjamin Mkapa, muda uliopangwa awali was aa 11:00 jioni na sis aa 1:00 usiku, leo Jumamosi, tarehe 8 Mei 2021. Anaripoti Kelvin Mwaipungu…(endelea).

Yanga wamesema, uamuzi wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), wa kubadili muda wa mtanange kati ya watani wa jadi, Simba dhidi ya Yanga, ni kinyume na Kanuni ya 15(10) za Ligi Kuu inayohusu taratibu za mchezo.

Kanuni hiyo inasema “mabadiliko yoyote ya muda wa kuanza mchezo yatajulishwa ipasavyo kwa pamnde zote husika za mchezo angalau saa 24 kabla ya muda wa awali.”

Hata hivyo, leo mchana Jumamosi, wakati mashabiki wakiwa tayari wameanza kuingia uwanjani, TFF ilitoa taarifa ya mabadiliko ya ratiba ya mchezo huo kwa kile ilichoeleza ni maelekezo kutoka Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo.

Taarifa hiyo ya TFF, haikufafanua zaidi sababu za msingi za mabadiliko ya mchezo huo.

Kutokana na hilo, taarifa ya Yanga, iliyotolewa na Idara ya Habari na Mawasiliano imesema “uongozi wa Yanga, unapinga mabadiliko hayo hivyo, itapeleka timu uwanjani kwa muda wa awali was aa 11:00 jioni.”

“Uongozi wa Yanga unaitaka Bodi ya Ligi na TFF kuendesha ligi kwa kuzingatia na kuheshimu kanuni zilizowekwa,” imesema Yanga

1 Comment

  • Ni woga wao tu mbona hata Ulaya huwa muda unabadirika lakini hakuna mbwembwe kama hizo wanazoonesha Yanga.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za SiasaTangulizi

Wakili Mwabukusi anusurika kufungiwa, asema hatarudi nyuma

Spread the loveWAKILI Boniface Mwabukusi amesema kuwa hatorudi nyuma kuwatetea Watanzania na...

Habari MchanganyikoHabari za SiasaTangulizi

Lissu akabidhiwa gari lake, aomba msaada wa matengenezo

Spread the loveMakamu Mwenyekiti wa Chadema Bara, Tundu Lissu leo Ijumaa amekabidhiwa...

Habari za SiasaTangulizi

Haya hapa majina walioteuliwa kugombea nafasi mbalimbali CHADEMA

Spread the loveCHAGUZI wa kanda za Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA)...

Habari MchanganyikoHabari za SiasaTangulizi

Uingereza yamwaga bil. 9 kumuunga mkono Samia matumizi nishati

Spread the loveWaziri Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira, Selemani...

error: Content is protected !!