Tuesday , 30 April 2024
Home Kitengo Michezo Simba, Yanga mageti kufungwa Saa 10
Michezo

Simba, Yanga mageti kufungwa Saa 10

Clifford Ndimbo, Msemaji wa TFF
Spread the love

 

IKIWA umebaki muda mchache kabla ya mtanange wa watani wa jadi Simba na Yanga, kupigwa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limetoa maelekezo ya kuwa mageti ya Uwanja yatafungwa saa 10:00 ikiwa ni saa moja kabla ya mchezo. Anaripoti Kelvin Mwaipungu, Dar es Salaam … (endelea).

Mchezo utapigwa leo majira ya saa 11 jioni kwenye Uwanja wa Benjamin Mkapa ambapo Simba atakuwa mwenyeji.

Akizungumza suala hilo, Afisa Habri wa TFF, Clifford Ndimbo amesema kwenye mchezo huu wa leo utaratibu utakuwa tofauti kwa kuwa mageti ya Uwanja huo yatafungwa saa moja kabla ya mchezo huo kuanza.

Aidha katika hatua nyingine Ndimbo alisema kwa kuwa mchezo huo umeangukia kipindi cha mwezi wa Ramadhan, wachezaji pamoja na mabenchi ya Ufundi yatapata muda wa kufuturu kwa mchezo kusimamishwa.

Alisema; “Wakati huu tupo kwenye mwezi wa Ramdhan na kuna wachezaji wapo kwenye mfungo kwa hiyo katika mchezo wa kesho kutakuwa na mapumziko mafupi ili kuwapa nafasi wachezaji na benchi la ufundi kupata futari.”

Kabla ya kuingia kwenye mchezo wa leo timu hizo zimekutana mara 107 kwenye mashindano yote, Simba imefanikiwa kuibuka na ushindi mara 32, huku Yanga ikishinda michezo 37 na wamefanikiwa kwenda sare mara 38.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoMichezo

Wanamichezo Mei Mosi wachangia wahitaji vitu vya mil. 11.5

Spread the loveWanamichezo wanaoshiriki Michezo ya Mei Mosi Taifa 2024 jijini Arusha...

Michezo

Usiku wa Ulaya umerejea kibabe kabisa

Spread the love  LIGI ya Mabingwa barani Ulaya imerejea tena na awamu...

Habari MchanganyikoMichezo

Mambo ya Ndani, Ulinzi zang’ara michezo ya Mei Mosi Arusha

Spread the loveRais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi nchini (TUCTA), Tumaini...

Michezo

Beti na Meridianbet mechi za leo

Spread the love IKIWA leo hii ni Jumapili tulivu kabisa, Meridianbet wanamkwambia...

error: Content is protected !!