Wednesday , 1 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Milioni 50 zamkamatishwa mfanyakazi Takukuru
Habari Mchanganyiko

Milioni 50 zamkamatishwa mfanyakazi Takukuru

Pingu
Spread the love

 

ZAINABU Mohamed Jabir, mtumishi wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), amekamatwa kwa tuhuma za kuomba na kupokea rushwa ya Sh.50 milioni. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Taarifa iliyotolewa na Doreen Kapwani, Msemaji wa Takukuru, leo Ijumaa, tarehe 30 Aprili 2021, imesema, Zainabu aliomba rushwa kutoka kwa mtu mmoja ili kumsaidia katika tuhuma dhidi yake, zinazochunguzwa na taasisi hiyo.

“Uchunguzi dhidi ya tuhuma hii unaendelea na utakapokamilika hatua stahiki zitachukuliwa,” amesema Doreen.

Afisa Uhusiano wa Takukuru, Doreen Kapwani

Taarifa hiyo ya Doreen, aliyoitoa kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu wa Takukuru, Brigedia Jenerali John Mbungo imetoa onyo kwa watu ambao wamekuwa wakijitambulisha kama watumishi wa taasisi hiyo.

Amesema, matapeli hao, wamekuwa wakiwapigia watu simu na kujitambulisha kwamba ni watumishi wa Takukuru kwamba wanapaswa kufika ofisini kuhojiwa, wakati si kweli.

Amewataka wananchi, wanapopokea simu za aina hiyo, kufika ofisi za Takukuru kujua ukweli zaidi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

NEMC yatoa elimu matumizi sahihi ya zebaki kwa wachimbaji

Spread the loveBARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC)...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Oryx gesi yagawa mitungi, majiko 100 kwa waandishi wa habari Dar

Spread the loveKAMPUNI ya Oryx Gesi Tanzania imegawa mitungi 100 ya gesi...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari MchanganyikoMichezo

Wanamichezo Mei Mosi wachangia wahitaji vitu vya mil. 11.5

Spread the loveWanamichezo wanaoshiriki Michezo ya Mei Mosi Taifa 2024 jijini Arusha...

error: Content is protected !!