Friday , 3 May 2024
Home Kitengo Michezo Kocha Dodoma Jiji: Tutaishangaza Simba kesho
Michezo

Kocha Dodoma Jiji: Tutaishangaza Simba kesho

Spread the love

 

KOCHA msaidizi wa kikosi cha Dodoma Jiji, Renatus Shija ameapa kuibuka na ushindi kwenye mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara dhidi ya Simba kesho kutokana na kuamini katika mbini zake. Anaripoti Kelvin Mwaipungu, Dar es Salaam … (endelea).

Mchezo huo wa Ligi Kuu utachezwa kesho kwenye Uwanja wa Benjamin Mkapa Jijini Dar es Salaam majira ya saa 1 usiku.

Akizungumza kwenye mkutano na waandishi wa Habari kocha huyo msaidizi amesema kuwa wamejipanga vizuri kukikabili Simba kesho licha ya kukili kuwa na kikosi kizuri kwa sasa.

“Tumejipanga vizuri kwa mchezo wa Simba kesho najua tupo Dar es Salaam na hapa ndiyo ngome yao kuu, lakini kuna kitu tumekiandaa tunataka tukawashangaze kesho ili tuondoke na pointi tatu katika mchezo huo,” alisema kocha huyo.

Timu hiyo inakwenda kucheza na Simba huku ikiwa imetoka kutoa sare kwenye mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara dhidi ya Azam FC mara baada ya kufungana mabao 2-2.

Kwa sasa Dodoma Jiji ipo nafasi ya sita kwenye msimamo huku ikiwa na pointi 38 mara baada ya kucheza michezo 27.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Europa na Conference kukupatia pesa ndefu leo

Spread the love  ALHAMISI ya leo tutaenda kushuhudia mitanange ya kukata na...

Habari MchanganyikoMichezo

Wanamichezo Mei Mosi wachangia wahitaji vitu vya mil. 11.5

Spread the loveWanamichezo wanaoshiriki Michezo ya Mei Mosi Taifa 2024 jijini Arusha...

Michezo

Usiku wa Ulaya umerejea kibabe kabisa

Spread the love  LIGI ya Mabingwa barani Ulaya imerejea tena na awamu...

Habari MchanganyikoMichezo

Mambo ya Ndani, Ulinzi zang’ara michezo ya Mei Mosi Arusha

Spread the loveRais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi nchini (TUCTA), Tumaini...

error: Content is protected !!