Saturday , 20 April 2024
Home Kitengo Michezo Kocha Dodoma Jiji: Tutaishangaza Simba kesho
Michezo

Kocha Dodoma Jiji: Tutaishangaza Simba kesho

Spread the love

 

KOCHA msaidizi wa kikosi cha Dodoma Jiji, Renatus Shija ameapa kuibuka na ushindi kwenye mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara dhidi ya Simba kesho kutokana na kuamini katika mbini zake. Anaripoti Kelvin Mwaipungu, Dar es Salaam … (endelea).

Mchezo huo wa Ligi Kuu utachezwa kesho kwenye Uwanja wa Benjamin Mkapa Jijini Dar es Salaam majira ya saa 1 usiku.

Akizungumza kwenye mkutano na waandishi wa Habari kocha huyo msaidizi amesema kuwa wamejipanga vizuri kukikabili Simba kesho licha ya kukili kuwa na kikosi kizuri kwa sasa.

“Tumejipanga vizuri kwa mchezo wa Simba kesho najua tupo Dar es Salaam na hapa ndiyo ngome yao kuu, lakini kuna kitu tumekiandaa tunataka tukawashangaze kesho ili tuondoke na pointi tatu katika mchezo huo,” alisema kocha huyo.

Timu hiyo inakwenda kucheza na Simba huku ikiwa imetoka kutoa sare kwenye mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara dhidi ya Azam FC mara baada ya kufungana mabao 2-2.

Kwa sasa Dodoma Jiji ipo nafasi ya sita kwenye msimamo huku ikiwa na pointi 38 mara baada ya kucheza michezo 27.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Anza Jumamosi yako na mkwanja wa Meridianbet

Spread the loveJumamosi ya leo ODDS zimekaa kijanja sana ndani ya Meridianbet...

Michezo

Tusua mkwanja na mechi za Ijumaa leo

Spread the love  LEO hii mechi zinaendelea kote na wewe kama unataka...

Michezo

Piga pesa na mechi za EUROPA leo hii

Spread the love Hatimaye Alhamisi ya EUROPA imefika ambapo leo hii mechi...

Michezo

Leo ni leo nani kutinga nusu fainali UEFA?

Spread the love HATIMAYE Jumanne ya UEFA imefika ambapo leo hii michezo...

error: Content is protected !!