Thursday , 30 March 2023
Home Kitengo Michezo Kocha Dodoma Jiji: Tutaishangaza Simba kesho
Michezo

Kocha Dodoma Jiji: Tutaishangaza Simba kesho

Spread the love

 

KOCHA msaidizi wa kikosi cha Dodoma Jiji, Renatus Shija ameapa kuibuka na ushindi kwenye mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara dhidi ya Simba kesho kutokana na kuamini katika mbini zake. Anaripoti Kelvin Mwaipungu, Dar es Salaam … (endelea).

Mchezo huo wa Ligi Kuu utachezwa kesho kwenye Uwanja wa Benjamin Mkapa Jijini Dar es Salaam majira ya saa 1 usiku.

Akizungumza kwenye mkutano na waandishi wa Habari kocha huyo msaidizi amesema kuwa wamejipanga vizuri kukikabili Simba kesho licha ya kukili kuwa na kikosi kizuri kwa sasa.

“Tumejipanga vizuri kwa mchezo wa Simba kesho najua tupo Dar es Salaam na hapa ndiyo ngome yao kuu, lakini kuna kitu tumekiandaa tunataka tukawashangaze kesho ili tuondoke na pointi tatu katika mchezo huo,” alisema kocha huyo.

Timu hiyo inakwenda kucheza na Simba huku ikiwa imetoka kutoa sare kwenye mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara dhidi ya Azam FC mara baada ya kufungana mabao 2-2.

Kwa sasa Dodoma Jiji ipo nafasi ya sita kwenye msimamo huku ikiwa na pointi 38 mara baada ya kucheza michezo 27.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

TANROADS wawataka watumishi wazingatie michezo kazini

Spread the love  WAKALA wa barabara Tanzania (TANROADS) imesema michezo inapaswa kuzingatiwa...

Michezo

Yanga: Fedha za Rais Samia zinaleta ari kubwa

Spread the loveUONGOZI wa klabu ya Yanga, umesema fedha zinazotolewa na Rais...

Michezo

Simba Sc. yamvulia kofia Rais Samia, yamuahidi makubwa dhidi ya Horoya

Spread the loveWAKATI timu ya Simba ikiibuka na ushindi wa bao 3-0...

Michezo

Taasisi ya TKO na TFF yawapiga msasa makocha wa kike 54

Spread the love WAKATI Soka la wasichana likichipua kwa kasi Taasisi ya...

error: Content is protected !!