Sunday , 19 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Vijiji vyote kufikishiwa umeme Desemba 2022
Habari Mchanganyiko

Vijiji vyote kufikishiwa umeme Desemba 2022

Spread the love

 

SERIKALI ya Tanzania, imesisitiza ifikapo Desemba 2022, vijiji vyote vya Tanzania Bara, vitakuwa vimefikishiwa umeme na Wakala wa Nishati Vijijini (REA). Anaripoti Jemima Samwel DMC … (endelea).

Kauli hiyo imetolewa leo Alhamisi, bungeni jijini Dodoma na Naibu Waziri wa Nishati, Steven Byabato, wakati akijibu swali la mbunge wa Bukoba Vijijini, Jasson Rwaikiza.

“Je, ni lini umeme utapelekwa katika Vijiji vya Buzi, Buguruka, Musina, Nsheshe na vingine ambavyo havijafikiwa na umeme katika Jimbo la Bukoba Vijijini,” amehoji Rweikiza

Akijibu swali hilo, Naibu Waziri Byabato amesema, Serikali kupitia REA, inaendelea kupeleka umeme na kufikisha katika vijiji vyote vya Tanzania Bara ifikapo Desemba, 2022.

“Vijiji vinane kati ya vijiji 94 vya Bukoba Vijijini ambavyo ni Buzi, Buguruka, Musira, Nsheshe, Ngarama, Omubweya, Kagarama na Rukoma vinatarajiwa kupatiwa umeme kupitia mradi wa REA awamu ya tatu mzunguko wa pili,” amesema Byabato

“Mradi huu ulianza kutekelezwa Machi, 2021 na unatarajia kukamilika Desemba, 2022. Gharama ya mradi ni Sh.2.04 bilioni,” amesema

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Balile aukwaa uenyekiti wahariri Afrika Mashariki

Spread the loveJumuiya ya Wahariri wa Afrika Mashariki (EAES), imemchagua Mwenyekiti wa...

Habari Mchanganyiko

Jeshi la Uhifadhi kujengewa uwezo zaidi

Spread the love  WIZARA ya Maliasili na Utalii imejipanga vyema kuendelea kulijengea...

Habari Mchanganyiko

Wanavyuo Dodoma waonja utamu wa chimbo la nyuki

Spread the love  TAMASHA la Chimbo la Nyuki lililofanyika katika Ukumbi wa...

Habari MchanganyikoHabari za SiasaTangulizi

Wakili Mwabukusi anusurika kufungiwa, asema hatarudi nyuma

Spread the loveWAKILI Boniface Mwabukusi amesema kuwa hatorudi nyuma kuwatetea Watanzania na...

error: Content is protected !!