Thursday , 2 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Natamani kurudi nyumbani – Lema
Habari za Siasa

Natamani kurudi nyumbani – Lema

Godbless Lema
Spread the love

 

GODBLESS Lema, aliyekuwa Mbunge wa Arusha Mjini (Chadema) ambaye kwa sasa anaishi uhamishoni Canada amesema, anatamani kurejea nyumbani. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam…(endelea).

Akizungumza katika moja ya Televisheni ya Mtandao, jana Jumatatu tarehe 19 Aprili 2020, Lema amesema atakapopata uthibitisho wa ulinzi wa maisha yake kutoka kwa mamlaka husika, atarejea nchini.

“Natamani kurudi nyumbani kushiriki sherehe za ndugu na rafiki zangu, lakini siwezi thubutu inaweza kuniletea maumivu makubwa, lakini mpaka pale nitakapopata uthibitisho wa uhakika kwamba, kuna haki na amani ya kutosha juu ya yangu.

“Experience (uzoefu) ngumu niliyonayo ya kwamba leo niko nje ya nyumbani nimeacha wazazi, rafiki na ndugu kwa kukimbia nchi. Ni experience mbaya sana, nisinge-wish (tamani) mwingine aipitie, hakuna experience mbaya kama umekimbia nyumbani halafu huji (hurudi) hata likizo,” amesema Lema.

Lema ambaye ni Mwenyekiti wa Chadema Kanda ya Kaskazini amesema, kwa sasa anamuomba Mungu ili Tanzania iendelee kuwa na amani na haki katika mihimili yake yote.

“Nafuatilia nyumbani kuliko mtu yoyote na naombea nyumbani kuliko mtu yoyote, kama kuna mtu pengine anayefanya sala kuona nyumbani pana badilika haraka na kuwa na amani na haki, kuanzia mahakama, polisi, bunge na serikali ni mimi,” amesema Lema.

Mwanasiasa huyo pamoja na familia yake, waliondoka nchini Tanzania Novemba 2020, kwa madai ya kupata vitisho vya usalama wake, baada ya uchaguzi mkuu.

Katika Uchaguzi Mkuu wa 2020, Lema aligombea Ubunge Arusha Mjini kupitia Chadema, na kuangushwa na Mrisho Gambo, aliyetangazwa mshindi wa jimbo hilo kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Lema aliungana na Lissu, aliyekuwa Mgombea Urais wa Tanzania kupitia Chadema katika uchaguzi huo,kuondoka nchini Tanzania kwa madai ya kuhofia usalama wa maisha yao.

Hata hivyo, zaidi ya mara mbili Insepekta Jenerali wa Polisi Tanzania (IGP), Simon Sirro aliwaita wanasiasa wote waliokimbia nchi warudi nchini, huku akiwahakikishia ulinzi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Spika Tulia aibana Serikali mafao ya wastaafu Jumuiya ya Afrika Mashariki

Spread the loveSPIKA wa Bunge, Dk. Tulia Ackson ameitaka Serikali kufanya tathimini...

Habari za Siasa

Serikali yawapa maagizo Ma-RC udhibiti magonjwa yasiyoambukiza

Spread the loveWAKUU wa mikoa nchini wametakiwa kuandaa utaratibu wa kuwawezesha wananchi...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari za Siasa

Mavunde aomba bilioni 231.9 bajeti wizara ya madini

Spread the loveWAZIRI wa Madini, Anthony Mavunde leo Jumanne amewasilisha hotuba ya...

error: Content is protected !!