Monday , 5 June 2023
Home Kitengo Maisha Elimu Serikali yatenga Mil 605 ukarabati Chuo Tango
Elimu

Serikali yatenga Mil 605 ukarabati Chuo Tango

Omary Kipanga, Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia
Spread the love

 

SERIKALI ya Tanzania inaendelea na ukarabati wa Chuo cha Maendeleo ya Wananchi, unaogharimu Sh. 605.2 milioni. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).

Kauli hiyo imetolewa na Omary Kipanga, Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia leo tarehe 20 Aprili 2021, akijibu swali la Flatei Gregori Massay, Mbunge wa Mbulu Vijijini (CCM), bungeni jijini Dodoma.

Massay ameuliza, “serikali ina mpango gani wa kujenga Chuo cha VETA katika Jimbo la Mbulu Vijijini ili vijana wapate ujuzi?”

Pipanga amesema, katika Wilaya ya Mbulu kuna Chuo cha Maendeleo ya Wananchi Tango, ambacho pia kinatoa mafunzo ya ufundi stadi.

“Chuo hiki, kinaendelea na ukarabati na ujenzi wa miundombinu, utakaogharimu jumla ya Tsh.605 milioni ambao unatarajiwa kukamilika Juni, 2021.”

“Hivyo, katika kipindi hiki ambacho serikali inaendelea na juhudi za kutafuta fedha kwa ajili ya ujenzi wa Chuo cha VETA wilayani humo, nashauri wananchi wa Jimbo la Mbulu Vijijini kuendelea kutumia vyuo vilivyopo nchini, ikiwa ni pamoja na Chuo Cha Maendeleo ya Wananchi- Tango na Chuo cha VETA Manyara,” amesema.

Amesema, serikali kupitia Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia ilitenga jumla ya Tsh.48.6 bilioni kwa ajili ya kujenga vyuo 29 vya VETA, katika ngazi ya wilaya ambavyo kwa sasa vipo katika hatua mbalimbali za ujenzi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Elimu

Serikali yatoa Sh. 573 mil. kukamilisha wa ujenzi sekondari ulioanzishwa na wanakijiji

Spread the love  SERIKALI kupitia Wizara ya Ofisi ya Rais-TAMISEMI, imetenga Sh....

Elimu

CBE yaja na kozi mpya 16 zikiwemo za ujasiriamali na uvumbuzi

Spread the loveChuo cha Elimu ya Biashara (CBE) kuanzia mwaka wa masomo...

Elimu

SUA kuhakikisha tafiti zinazofanywa zisiachwe kwenye makabati

Spread the love  MRATIBU wa utafiti na machapisho katika kurugenzi ya uzamiri,...

Elimu

Watakaopata Division One St Anne Marie Academy kupewa iphone ya macho matatu

Spread the loveMkurugenzi wa shule za St Anne Marie Academy, Dk. Jasson...

error: Content is protected !!