Saturday , 25 March 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Rais Samia ateua viongozi nane
Habari za Siasa

Rais Samia ateua viongozi nane

Samia Suluhu Hassan, Rais wa Tanzania
Spread the love

 

RAIS wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, amefanya uteuzi wa viongozi mbalimbali nane. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).

Taarifa iliyotolewa na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, Ikulu Gerson Msigwa leo Jumatatu, tarehe 19 Aprili 2021, imewataja viongozi walioteuliwa kuwa ni;

1. Amemteua Dk. Richard J. Masika kuwa Mwenyekiti wa Baraza la Taasisi ya Teknolojia Dar es Salaam (DIT).

Uteuzi huo umeanza tarehe 16 Aprili, 2021. Dk. Masika anachukua nafasi ya marehemu Prof. Apollinary Elikana Peleka.

2. Amemteua Prof. Joseph J. Msambichaka kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Tume ya Nguvu za Atomiki Tanzania (TAEC).

Ueuzi huo umeanza tarehe 15 Aprili, 2021. Prof. Msambichaka anachukua nafasi ya Prof. Manase Peter Salema.

3. Amemteua Dk. Revocatus Petro Mushumbusi kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Utafiti wa Misitu Tanzania (TAFORI).

Uteuzi huu umeanza tarehe 16 Aprili, 2021. Dk. Mshumbusi anachukua nafasi iliyoachwa wazi na Dk. Ladislaus Nshubemuki ambaye amestaafu.

4. Amemteua Prof. John W.A. Kondoro kuendelea kuwa Mwenyekiti wa Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi (NACTE), baada ya kumaliza muda wa kipindi cha kwanza. Uteuzi huu umeanza tarehe 15 Aprili, 2021.

5. Amemteua Dk. Mboni A. Ruzegea kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Huduma za Maktaba Tanzania (TLSB).

Uteuzi huu umeanza tarehe 16 Aprili, 2021. Dk. Ruzegea anachukua nafasi iliyoachwa wazi na Dk. Ali Mcharazo ambaye amestaafu.

6. Amemteua Prof. Esther Hellen Lugwisha kuendelea kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali baada ya kumaliza muda wa kipindi cha kwanza. Uteuzi huu umeanza tarehe 15 Aprili, 2021.

7. Amemteua Kept. Ernest Mihayo Bupamba kuendelea kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Chuo cha Bahari Dar es Salaam (Dar es Salaam Maritime Institute – DMI) baada ya kumaliza kipindi cha kwanza. Uteuzi huu umeanza tarehe 15 Aprili, 2021.

8. Amememteua Prof. Makenya Maboko kuendelea kuwa Mwenyekiti wa Kamisheni ya Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH) baada ya kumaliza muda wa kipindi cha kwanza. Uteuzi huu umeanza tarehe 15 Aprili, 2021.

1 Comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Rais Samia aagiza iundwe kamati ya pamoja ya Mawaziri mradi wa BBT

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amewaagiza mawaziri kuunda kamati...

Habari za Siasa

Rais Samia apangua makatibu tawala mikoa, ateua Kamishna DCEA

Spread the loveALIYEKUWA Kamishna wa Mamlaka ya Kudhibiti Dawa za Kulevya, Gerald...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

M/kiti bodi ya wadhamini Chadema afariki dunia

Spread the loveMWENYEKITI wa Bodi ya Wadhamini ya Chama cha Demokrasia na...

Habari za Siasa

Zitto: Nikifa Ado atavaa viatu vyangu

Spread the love  KIONGOZI Mkuu wa Chama cha ACT Wazalendo, Zitto Kabwe...

error: Content is protected !!