Saturday , 27 April 2024
Home Habari Mchanganyiko “Mchuano mkali uchaguzi TLS”
Habari Mchanganyiko

“Mchuano mkali uchaguzi TLS”

Dk. Rugemeleza Nshala
Spread the love

 

RAIS wa Chama cha Wanasheria wa Tanganyika (TLS), anayemaliza muda wake, Dk. Lugemeleza Nshala amesema, uchaguzi wa viongozi wa chama hicho 2021, umezungukwa na mchuano mkali, ikilinganishwa na chaguzi zilizopita. Anaripoti Regina Mkonde, Arusha … (endelea).

Dk. Nshala ametoa kauli hiyo leo Jumatano tarehe 14 Aprili 2021, wakati anazungumza na MwanaHALISI Online jijini Arusha.

TLS kinatarajia kufanya uchaguzi wa rais, makamu wa rais na mweka hazina, Ijumaa tarehe 16 Aprili 2021.

Akizungunzia uchaguzi huo, Dk. Nshala amesema, mchuano huo ni mkali kwa kuwa wagombea wake wana ushawishi mkubwa, sambamba na uchaguzi huo kufuatiliwa na watu wengi nchini.

“Sasa kuna mchuano mkali,  inaonesha TLS ina umihumu sana katika kuhakikisha nchi inaongozwa kwa misingi ya sheria,” amesema Dk. Nshala.

Dk. Edward Hoseah, mgombea Urais TLS

Wanaochuana kurithi mikoba ya Dk. Nshala ni, Dk. Edward Hoseah, Flaviana Charles, Shehzada Walli, Francis Stolla na Albert Msando.

Kauli hiyo ya Dk. Nshala imekuja katika kipindi cha lala salama, ambapo kampeni zake zinatarajiwa kufungwa kesho Alhamisi tarehe 15 Aprili 2021.

Mbali na uchaguzi wa viongozi wa ngazi za juu, TLS leo kimefanya uchaguzi wa viongozi wa kanda na wa chama cha wanasheria vijana.

Viongozi watakaoshinda katika chaguzi hizo, wataapishwa Jumamosi tarehe 17 Aprili 2021.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Mvungi aendesha kikao kazi cha wataalam wa Regrow

Spread the love  MKURUGENZI wa Idara Sera na Mipango Wizara ya Maliasili...

Habari MchanganyikoTangulizi

Jacob, Malisa waachiwa kwa masharti

Spread the love  JESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam,...

Habari Mchanganyiko

Polisi wakanusha kufanya uzembe ajali iliyouwa mwandishi Ayo Tv

Spread the loveJESHI la Polisi limekanusha tuhuma zilizoibuliwa dhidi yake  kwamba limekawia...

Habari Mchanganyiko

Rais Samia kuzindua gazeti litakalotoa habari za wafanyakazi Tanzania

Spread the loveSHIRIKISHO la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA), liko mbioni kufufua...

error: Content is protected !!