Thursday , 28 March 2024
Home Habari Mchanganyiko “Mchuano mkali uchaguzi TLS”
Habari Mchanganyiko

“Mchuano mkali uchaguzi TLS”

Dk. Rugemeleza Nshala
Spread the love

 

RAIS wa Chama cha Wanasheria wa Tanganyika (TLS), anayemaliza muda wake, Dk. Lugemeleza Nshala amesema, uchaguzi wa viongozi wa chama hicho 2021, umezungukwa na mchuano mkali, ikilinganishwa na chaguzi zilizopita. Anaripoti Regina Mkonde, Arusha … (endelea).

Dk. Nshala ametoa kauli hiyo leo Jumatano tarehe 14 Aprili 2021, wakati anazungumza na MwanaHALISI Online jijini Arusha.

TLS kinatarajia kufanya uchaguzi wa rais, makamu wa rais na mweka hazina, Ijumaa tarehe 16 Aprili 2021.

Akizungunzia uchaguzi huo, Dk. Nshala amesema, mchuano huo ni mkali kwa kuwa wagombea wake wana ushawishi mkubwa, sambamba na uchaguzi huo kufuatiliwa na watu wengi nchini.

“Sasa kuna mchuano mkali,  inaonesha TLS ina umihumu sana katika kuhakikisha nchi inaongozwa kwa misingi ya sheria,” amesema Dk. Nshala.

Dk. Edward Hoseah, mgombea Urais TLS

Wanaochuana kurithi mikoba ya Dk. Nshala ni, Dk. Edward Hoseah, Flaviana Charles, Shehzada Walli, Francis Stolla na Albert Msando.

Kauli hiyo ya Dk. Nshala imekuja katika kipindi cha lala salama, ambapo kampeni zake zinatarajiwa kufungwa kesho Alhamisi tarehe 15 Aprili 2021.

Mbali na uchaguzi wa viongozi wa ngazi za juu, TLS leo kimefanya uchaguzi wa viongozi wa kanda na wa chama cha wanasheria vijana.

Viongozi watakaoshinda katika chaguzi hizo, wataapishwa Jumamosi tarehe 17 Aprili 2021.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga kuongoza usambazaji wa mitungi ya gesi 10,000 ya Taifa Gas

Spread the loveNaibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga ameahidi kuongoza kwa ufanisi...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wafanyabiashara, wawekezaji China waridhia kuwekeza bil. 800 katika sekta 5 nchini

Spread the loveUJUMBE wa wafanyabiashara na wawekezaji wakubwa kutoka Jimbo la Changzhou...

Habari Mchanganyiko

Bil. 4.42 kumaliza uhaba maji kata 2 Musoma Vijijini

Spread the loveWANANCHI wa kata za Busambara na Kiriba, Jimbo la Musoma...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Soko nepi za watoto lashuka, watu wazima lapaa

Spread the loveKiwanda cha kutengeneza nepi cha Japan kimetangaza kuwa kitaacha kutengeneza...

error: Content is protected !!