Tuesday , 19 March 2024
Home Habari Mchanganyiko “Mchuano mkali uchaguzi TLS”
Habari Mchanganyiko

“Mchuano mkali uchaguzi TLS”

Dk. Rugemeleza Nshala
Spread the love

 

RAIS wa Chama cha Wanasheria wa Tanganyika (TLS), anayemaliza muda wake, Dk. Lugemeleza Nshala amesema, uchaguzi wa viongozi wa chama hicho 2021, umezungukwa na mchuano mkali, ikilinganishwa na chaguzi zilizopita. Anaripoti Regina Mkonde, Arusha … (endelea).

Dk. Nshala ametoa kauli hiyo leo Jumatano tarehe 14 Aprili 2021, wakati anazungumza na MwanaHALISI Online jijini Arusha.

TLS kinatarajia kufanya uchaguzi wa rais, makamu wa rais na mweka hazina, Ijumaa tarehe 16 Aprili 2021.

Akizungunzia uchaguzi huo, Dk. Nshala amesema, mchuano huo ni mkali kwa kuwa wagombea wake wana ushawishi mkubwa, sambamba na uchaguzi huo kufuatiliwa na watu wengi nchini.

“Sasa kuna mchuano mkali,  inaonesha TLS ina umihumu sana katika kuhakikisha nchi inaongozwa kwa misingi ya sheria,” amesema Dk. Nshala.

Dk. Edward Hoseah, mgombea Urais TLS

Wanaochuana kurithi mikoba ya Dk. Nshala ni, Dk. Edward Hoseah, Flaviana Charles, Shehzada Walli, Francis Stolla na Albert Msando.

Kauli hiyo ya Dk. Nshala imekuja katika kipindi cha lala salama, ambapo kampeni zake zinatarajiwa kufungwa kesho Alhamisi tarehe 15 Aprili 2021.

Mbali na uchaguzi wa viongozi wa ngazi za juu, TLS leo kimefanya uchaguzi wa viongozi wa kanda na wa chama cha wanasheria vijana.

Viongozi watakaoshinda katika chaguzi hizo, wataapishwa Jumamosi tarehe 17 Aprili 2021.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Diwani, wananchi wengine 463 wahama Ngorongoro

Spread the loveMakamu mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Ngorongoro ambaye pia...

ElimuHabari Mchanganyiko

GGML yawapa mbinu wanafunzi Geita Boys kufikia malengo ya kitaaluma

Spread the loveKampuni ya Geita Gold Mining Limited (GGML) imetoa mafunzo maalumu...

Habari MchanganyikoKimataifa

Shule zafungwa kutokana na ongezeko la joto

Spread the loveSUDAN Kusini imeamuru kufungwa kwa shule zote kuanzia leo Jumatatu,...

Habari Mchanganyiko

Bunge laja na Marathon kuchangia ujenzi wa sekondari

Spread the loveBUNGE la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania linatarajia kukusanya fedha...

error: Content is protected !!