Sunday , 28 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mto Ruvuma kuzalisha umeme
Habari za Siasa

Mto Ruvuma kuzalisha umeme

Mto Ruvuma
Spread the love

 

MAJI ya Mto Ruvuma, yapo kwenye mpango wa serikali kutumika kuzalisha umeme. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).

Kauli hiyo imetolewa na Jumaa Aweso, Waziri wa Maji leo Jumatatu tarehe 12 Aprili 2021, bungeni jijini Dodoma, wakati akijibu swali la Abdallah Chikota, Mbunge wa Nanyamba (CCM), aliyetaka kujua mpango wa serikali kuhusu hilo.

Chikota ameuliza, ni lini serikali itaanza kutumia maji ya Mto Ruvuma kwa ajili ya kujenga miradi mikubwa ya maji, ambayo itatatua changamoto za maji kwa Jimbo la Nanyamba na maeneo Jirani?

“Mradi wa maji kutoka Mto Ruvuma ni miongoni mwa miradi mikubwa ya kimkakati, serikali inatarajia kuanza utekelezaji wake katika mwaka wa fedha 2021/22 kulingana na upatikanaji wa fedha.

Juma Aweso, Waziri wa Maji

“Kupitia RUWASA, ukarabati na upanuzi wa mradi wa maji kwenye vijiji vya Malongo na Migombani umekamilika na unatoa huduma kwa wananchi, Vilevile, visima viwili (2) vimechimbwa, mtambo nyumba ya mitambo ya kusukuma maji, ulazaji wa bomba kuu kilomita 3.5.

“Ujenzi wa tanki moja (1) la ujazo wa lita 100,000 na ujenzi wa matanki mengine manne (4) unaendelea,” amesema waziri huo.

Amesema, utekelezaji wa miradi katika vijiji vya Ngonja – Chawi, Mayembejuu, Nyundo A na B, Nitekela na Misufini upo katika hatua mbalimbali za utekelezaji.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Biteko aipongeza GGML kudhibiti vifo, majeruhi mahali pa kazi

Spread the loveNAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

Habari za Siasa

Askofu Shoo awataka ACT kupigania maslahi ya Taifa, wasikubali kuhongwa

Spread the loveALIYEKUWA Askofu Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri, Askofu...

Habari za Siasa

Biteko aagiza waajiri kudhibiti vifo mahali pa kazi

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde aibana kampuni kutimiza masharti ya mkataba

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameitaka Kampuni ya Xin Tai...

error: Content is protected !!