Thursday , 30 March 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Mto Ruvuma kuzalisha umeme
Habari za Siasa

Mto Ruvuma kuzalisha umeme

Mto Ruvuma
Spread the love

 

MAJI ya Mto Ruvuma, yapo kwenye mpango wa serikali kutumika kuzalisha umeme. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).

Kauli hiyo imetolewa na Jumaa Aweso, Waziri wa Maji leo Jumatatu tarehe 12 Aprili 2021, bungeni jijini Dodoma, wakati akijibu swali la Abdallah Chikota, Mbunge wa Nanyamba (CCM), aliyetaka kujua mpango wa serikali kuhusu hilo.

Chikota ameuliza, ni lini serikali itaanza kutumia maji ya Mto Ruvuma kwa ajili ya kujenga miradi mikubwa ya maji, ambayo itatatua changamoto za maji kwa Jimbo la Nanyamba na maeneo Jirani?

“Mradi wa maji kutoka Mto Ruvuma ni miongoni mwa miradi mikubwa ya kimkakati, serikali inatarajia kuanza utekelezaji wake katika mwaka wa fedha 2021/22 kulingana na upatikanaji wa fedha.

Juma Aweso, Waziri wa Maji

“Kupitia RUWASA, ukarabati na upanuzi wa mradi wa maji kwenye vijiji vya Malongo na Migombani umekamilika na unatoa huduma kwa wananchi, Vilevile, visima viwili (2) vimechimbwa, mtambo nyumba ya mitambo ya kusukuma maji, ulazaji wa bomba kuu kilomita 3.5.

“Ujenzi wa tanki moja (1) la ujazo wa lita 100,000 na ujenzi wa matanki mengine manne (4) unaendelea,” amesema waziri huo.

Amesema, utekelezaji wa miradi katika vijiji vya Ngonja – Chawi, Mayembejuu, Nyundo A na B, Nitekela na Misufini upo katika hatua mbalimbali za utekelezaji.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

TEMESA iliyokarabati Kivuko kwa Bil 7.5 yapata hati chafu

Spread the love  MDHIBITI na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG),...

Habari za Siasa

ACT-Wazalendo yakusanya Mil 8.5/- kodi ya zuio na kutokomea nazo

Spread the love  MDHIBITI na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG),...

Habari za Siasa

DC Kasilda Mgeni ahamasisha chakula shuleni

Spread the love  MKUU wa Wilaya ya Same, mkoani Kilimanjaro, Kasilda Mgeni...

Habari za Siasa

Bilioni 223.9 zapelekwa Tunduru ndani ya miaka 2 ya SSH

Spread the love  ZAIDI ya Sh. bilioni 223.9 zimepelekwa Wilaya ya Tunduru...

error: Content is protected !!