Thursday , 28 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mto Ruvuma kuzalisha umeme
Habari za Siasa

Mto Ruvuma kuzalisha umeme

Mto Ruvuma
Spread the love

 

MAJI ya Mto Ruvuma, yapo kwenye mpango wa serikali kutumika kuzalisha umeme. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).

Kauli hiyo imetolewa na Jumaa Aweso, Waziri wa Maji leo Jumatatu tarehe 12 Aprili 2021, bungeni jijini Dodoma, wakati akijibu swali la Abdallah Chikota, Mbunge wa Nanyamba (CCM), aliyetaka kujua mpango wa serikali kuhusu hilo.

Chikota ameuliza, ni lini serikali itaanza kutumia maji ya Mto Ruvuma kwa ajili ya kujenga miradi mikubwa ya maji, ambayo itatatua changamoto za maji kwa Jimbo la Nanyamba na maeneo Jirani?

“Mradi wa maji kutoka Mto Ruvuma ni miongoni mwa miradi mikubwa ya kimkakati, serikali inatarajia kuanza utekelezaji wake katika mwaka wa fedha 2021/22 kulingana na upatikanaji wa fedha.

Juma Aweso, Waziri wa Maji

“Kupitia RUWASA, ukarabati na upanuzi wa mradi wa maji kwenye vijiji vya Malongo na Migombani umekamilika na unatoa huduma kwa wananchi, Vilevile, visima viwili (2) vimechimbwa, mtambo nyumba ya mitambo ya kusukuma maji, ulazaji wa bomba kuu kilomita 3.5.

“Ujenzi wa tanki moja (1) la ujazo wa lita 100,000 na ujenzi wa matanki mengine manne (4) unaendelea,” amesema waziri huo.

Amesema, utekelezaji wa miradi katika vijiji vya Ngonja – Chawi, Mayembejuu, Nyundo A na B, Nitekela na Misufini upo katika hatua mbalimbali za utekelezaji.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

error: Content is protected !!